Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kuacha Mambo ya Teknolojia pa Nafasi Yake

Namna ya Kuacha Mambo ya Teknolojia pa Nafasi Yake

 Kutumia mambo ya teknolojia inaweza kufanya ndoa ikuwe nguvu ao iharibike. Hali iko namna gani mu ndoa yenu?

 Mambo yenye unapaswa kujua

  •   Kutumia muzuri mambo ya teknolojia, sawa vile telefone, kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri mu ndoa. Kwa mufano, bwana na bibi fulani wanaitumia juu ya kupashana habari muchana wakati hawako fasi moja.

     “Kutumiana tu sms yenye kusema ‘Nakupenda’ ao ‘Niko nakuwaza’ kunaweza kufanya weye na bibi yako mujisikie kuwa karibu sana.”​—Jonathan.

  •   Kutumia mubaya mambo ya teknolojia kunaweza kuharibisha ndoa. Kwa mufano, watu fulani wanatumiaka telefone ao tablete zao kila wakati, ile inafanya wasikuwe na wakati wa kuhangaikia bibi ao bwana yao.

     “Niko hakika kama kulikuwa wakati bwana yangu angependa kuzungumuza na miye kama singekuwa natumikisha telefone yangu.”​—Julissa.

  •   Watu fulani wanasema kama wanaweza kuzungumuza muzuri na bibi ao bwana yao hata kama wako wanatumikisha telefone ao tablete yao. Sherry Turkle, mwanamuke fulani mwenye elimu ya sociolojia alionyesha kama ile haiwezekane. Ni wazi kama, hata ikiwa watu wanawaza kama wako na uwezo wa kufanya mambo ya mingi kwa wakati moja, ile haiko jambo ya muzuri. Sherry anasema kama, kwa kweli, ‘kadiri tunajikaza kufanya mambo ya mingi wakati ileile, ni vile tunashindwa kuifanya muzuri.’ a

     “Napendaka sana kuzungumuza na bwana yangu, lakini hapana wakati iko anazungumuza na miye na wakati ileile iko anafanya mambo ingine, sawa vile kutumikisha telefone. Akifanya vile naonaka kama hanihangaikie.”​—Sarah.

 Wazo kubwa: Namna unatumia mambo ya teknolojia, sawa vile telefone ao tablete, inaweza kusaidia ao kuharibu ndoa yako.

 Mambo yenye unaweza kufanya

 Jua mambo ya kutia pa nafasi ya kwanza. Biblia inasema: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.” (Wafilipi 1:10) Ujiulize, ‘Mambo ya teknolojia inatuibaka wakati miye na bibi yangu; wakati yenye tungetumia ili kuzungumuza?’

 “Inahuzunisha sana kuona bibi na bwana wako wanatumia chakula ku restaurant lakini ileile wakati kila mumoja wao iko anatumia telefone yake. Hatupendi kuwa watumwa wa mambo ya teknolojia na kusahau mambo ya maana zaidi, ni kusema, uhusiano kati yetu.”​—Matthew.

 Ujiwekee mipaka. Biblia inasema: “Muendelee kuwa waangalifu sana ili namna munatembea isikuwe kama watu wenye hawana hekima lakini kama watu wenye hekima, mukitumia muzuri zaidi wakati wenu.” (Waefeso 5:15, 16) Ujiulize, ‘Naweza kujiwekea wakati wa kusoma na kujibia ujumbe zenye haziko za haraka sana, kuliko kujibia palepale kila ujumbe wakati tu inafika?’

 “Nimeona kama ni muzuri kutia telefone yangu mu hali yenye haitatoa sauti na kisha kujibia ma sms yote yenye nimepata wakati wenye kufaa. Ni jambo yenye haitokee sana kuitwa, kupata sms ao ujumbe ku Enternete wenye kuomba jibu la haraka sana.”​—Jonathan.

 Ikiwezekana, fanya mambo ya kazi ku kazi tu. Biblia inasema: “Kila kitu kiko na wakati wake wenye uliwekwa.” (Muhubiri 3:1) Ujiulize: ‘Natumikishaka telefone juu ya kufanya mambo ya kazi wakati niko kunyumba? Kama ni vile, ile iko na matokeo gani juu ya familia yangu? Bibi ao bwana yangu anaweza kujibia namna gani ile ulizo?’

 “Juu ya mambo ya teknolojia, tunaweza kuendelea kutumika saa ni saa. Niko najikaza kuacha kutumia kila wakati telefone yangu na kuacha kufanya mambo ya kazi wakati niko pamoja na bibi yangu.”​—Matthew.

 Muzungumuze pamoja kuhusu namna ya kutumia mambo ya teknolojia. Biblia inasema: “Kila mumoja aendelee kutafuta, hapana faida yake mwenyewe, lakini faida ya ule mutu mwingine.” (1 Wakorinto 10:24) Zungumuza na bibi ao bwana yako juu ya namna kila mumoja wenu anatumiaka mambo ya teknolojia, na kama ni lazima, ni mabadiliko gani anaweza kufanya. Wakati wa ile mazungumuzo, munaweza kuanza kwa kutumia sehemu maulizo ya kufikiria sana, yenye kuwa mu hii habari.

 “Miye na bwana yangu tunaambianaka mambo waziwazi wakati mumoja wetu anaanza kutumia tablete ao telefone yake sana. Siye wawili tunajua kama ile inaweza kuleta shida, kwa hiyo, tunafikiria kwa uangalifu mawazo ya kila mumoja wetu.”​—Danielle.

 Wazo kubwa: Hakikisha kama hauyakuwa mutumwa wa mambo ya teknolojia.

a Ona kitabu Reclaiming Conversation​—The Power of Talk in a Digital Age.