Ona video zinazopatikana

Namna Gani Naweza Kupata Dini ya Kweli?

Namna Gani Naweza Kupata Dini ya Kweli?

Jibu la Biblia

 Ili kuonyesha tofauti kati ya watu wenye kuwa katika dini ya kweli na wenye kuwa katika dini ya uongo, Biblia inasema hivi: ‘Kwa matunda yao mutawatambua. Je, watu hukusanya zabibu kutoka kwenye miiba au tini kutoka kwenye michongoma?’ (Mathayo 7:16) Kama vile tu unaweza kutofautisha muzabibu na muti wa miiba kupitia matunda yake, unaweza pia kutofautisha dini ya kweli na dini ya uongo kupitia matunda yake, ao kupitia alama zenye kufuata.

  1.   Dini ya kweli inafundisha kweli yenye kutegemea Biblia, hapana mawazo ya watu. (Yohana 4:24; 17:17) Hilo linatia ndani ukweli kuhusu nafsi na tumaini la uzima wa milele katika paradiso duniani. (Zaburi 37:29; Isaya 35:5, 6; Ezekieli 18:4) Tena haigope kufunua waziwazi uongo wa dini.—Mathayo 15:9; 23:27, 28.

  2.   Dini ya kweli inasaidia watu kumujua Mungu, na inawafundisha pia jina lake, Yehova. (Zaburi 83:18; Isaya 42:8; Yohana 17:3, 6) Kuliko kufundisha kwamba Mungu haeleweke wala hapendezwe na watu, dini ya kweli inafundisha kwamba Mungu anataka tukuwe na uhusiano pamoja naye.—Yakobo 4:8.

  3.   Dini ya kweli inafundisha kwamba Yesu Kristo ndiye njia moja tu yenye Mungu anatumia ili kuokoa wanadamu. (Matendo 4:10, 12) Washiriki wa dini ya kweli wanatii amri za Yesu na wanajikaza kufuata mufano wake.—Yohana 13:15; 15:14

  4.   Dini ya kweli inaona Ufalme wa Mungu tu kuwa tumaini la wanadamu. Washiriki wa dini ya kweli wanatangazia wengine kwa bidii kuhusu Ufalme.—Mathayo 10:7; 24:14.

  5.   Dini ya kweli inatia watu moyo kupendana bila uchoyo. (Yohana 13:35) Inafundisha washiriki wake kuheshimu watu wa makabila yote na inakaribisha watu wa rangi, luga, na desturi zote. (Matendo 10:34, 35) Kwa sababu ya upendo, washiriki wa dini ya kweli hawaende katika vita.—Mika 4:3; 1 Yohana 3:11, 12

  6.   Dini ya kweli haina viongozi wenye kupokea mushahara, na hakuna washiriki wake wenye wanapewa majina ya cheo.—Mathayo 23:8-12; 1 Petro 5:2, 3

  7.   Dini ya kweli haiunge mukono upande wowote katika mambo ya siasa. (Yohana 17:16; 18:36) Lakini, washiriki wake wanaheshimu na kutii serikali ya inchi yao, kulingana na amri hii ya Biblia: ‘Mulipeni Kaisari vitu vya Kaisari [ni kusema wenye mamlaka], lakini Mungu vitu vya Mungu.’—Marko 12:17; Waroma 13:1, 2

  8.   Dini ya kweli ni njia ya maisha, si kufuata mambo kidesturi tu. Washiriki wake wanashika sana kanuni za juu za mwenendo katika kila sehemu ya maisha. (Waefeso 5:3-5; 1 Yohana 3:18) Kuliko kufikiri kwamba wamenyimwa furaha, washiriki wa dini ya kweli wanapata furaha ya kuabudu “Mungu mwenye furaha.”—1 Timotheo 1:11.

  9.   Wale wenye kuwa katika dini ya kweli ni wadogo. (Mathayo 7:13, 14) Mara nyingi, washiriki wa dini ya kweli wanazarauliwa, wanazihakiwa, na kuteswa kwa sababu ya kufanya mapenzi ya Mungu.—Mathayo 5:10-12.

Dini ya kweli haiko tu ‘dini yenye tunapenda’

 Kuko hatari ya kuchagua dini kwa kutegemea tu namna tunajisikia kuhusu dini hiyo. Biblia ilitabiri wakati wenye watu “watajikusanyia walimu [wa dini] kwa ajili yao wenyewe ili masikio yao yafurahishwe.” (2 Timotheo 4:3) Tofauti na hilo, Biblia inatutia moyo tufuate “ibada iliyo safi na isiyotiwa unajisi kwa maoni ya Mungu wetu na Baba,” hata kama ni dini yenye watu wengi hawapende.—Yakobo 1:27; Yohana 15:18, 19.