Ona video zinazopatikana

Nafsi Ni Nini?

Nafsi Ni Nini?

Jibu ya Biblia

 Neno “nafsi” yenye inapatikana mu Biblia inatokana na neno ya Kiebrania neʹphesh na neno ya Kigiriki psy·kheʹ. Wakati neno neʹphesh inatafsiriwa neno kwa neno, inamaanisha “kiumbe yenye kupumua,” na neno ya Kigiriki psy·kheʹ inamaanisha “kiumbe yenye uzima.” * Kwa hiyo, nafsi haiko kitu yenye kuwa ndani ya mwili, yenye inaendeleaka kuishi kisha mwili kufa. Ona namna Biblia inaonyesha kama nafsi ni mutu kwa ujumla.

Adamu hakupewa nafsi​—‘Alikuwa nafsi yenye uzima’

  •   Wakati Yehova Mungu aliumba mutu wa kwanza, Adamu, Biblia inasema kama “akakuwa nafsi [yenye] uzima.” (Mwanzo 2:7, maelezo ya chini) Biblia haiseme kama Adamu alipewa nafsi, inasema akakuwa nafsi, ao mutu mwenye uzima.

  •   Biblia inasema kama nafsi inaweza kutumika, kusikia njala, kukula, kutii sheria, na kugusa maiti. (Mambo ya Walawi 5:2; 7:20; 23:30; Kumbukumbu la Torati 12:20; Waroma 13:1) Mutu njo anaweza kufanya ile mambo.

Nafsi inaweza kufa?

 Ndiyo. Kuko maandiko mingi ya Biblia yenye inaonyesha kama nafsi inakufaka. Ona mifano fulani:

  •   “Nafsi yenye inatenda zambi ndiyo itakufa.”​—Ezekieli 18:4, 20.

  •   Mu Israeli ya zamani, kama mutu angefanya zambi nzito, ‘nafsi [yake] ilipaswa kuondolewa.’ (Kutoka 12:15, 19; Mambo ya Walawi 7:20, 21, 27; 19:8) Ni kusema ule mutu alipaswa “kuuawa.”​—Kutoka 31:14, maelezo ya chini.

  •   Kisha mutu kufa, maneno “nafsi yenye imekufa” inatumiwa mu maandiko fulani juu ya kuzungumuzia maiti. (Mambo ya Walawi 21:11, maelezo ya chini; Hesabu 6:6, maelezo ya chini) Hata kama tafsiri fulani za Biblia zinatumia maneno “mwili wenye kufa” ao “mutu mwenye kufa” mu ile maandiko, maandishi ya Kiebrania inatumia neno neʹphesh, ni kusema “nafsi.”

Neno “nafsi” inaweza kumaanisha “uzima”

 Biblia inatumia pia neno “nafsi” ili kumaanisha “uzima.” Kwa mufano, mu Yobu 33:22, neno ya Kiebrania yenye kutafsiriwa “nafsi,” ni kusema neʹphesh inatumiwa ili kumaanisha “uzima.” Vilevile, Biblia inaonyesha kama nafsi ya mutu, ao uzima wa mutu, unaweza kuwa mu hatari ao kupotea.​—Kutoka 4:19; Waamuzi 9:17; Wafilipi 2:30.

 Ile matumizi ya neno “nafsi” inatusaidia kuelewa maandiko yenye inasema kama nafsi “ilikuwa inatoka.” (Mwanzo 35:18, maelezo ya chini) Ile maneno ya mufano inaonyesha kama uzima wa mutu ulikuwa unafikia mwisho wake. Tafsiri fulani zinasema hivi mu Mwanzo 35:18: “Alipumua pumuzi yake ya mwisho.”

Fundisho ya kutokufa kwa nafsi ilitoka wapi?

 Dini za Kikristo zenye zinaamini kama nafsi haikufake zilitosha ile fundisho mu filozofia ya Wagiriki, hapana mu Biblia. Kitabu Encyclopædia Britannica inasema kama mu Biblia, neno nafsi inamaanisha kitu fulani yenye kupumua, haiko kitu fulani yenye haionekane yenye iko tofauti na mwili. Inasema pia kama ni kwa Wagiriki wa zamani njo makanisa ilitosha wazo yenye kuonyesha kama nafsi iko tofauti na mwili.

 Mungu hapendi tuchange mafundisho yake na filozofia za wanadamu, sawa vile fundisho yenye kuonyesha kama nafsi haikufake. Biblia inatuonya hivi: “Mufanye angalisho ili mutu yeyote asiwakamate mateka kupitia filozofia na udanganyifu wa bure kulingana na desturi ya wanadamu, kulingana na mambo ya musingi ya ulimwengu na hapana kulingana na Kristo.”​—Wakolosai 2:8.

^ Ona The New Brown, Driver, and Briggs Hebrew and English Lexicon of the Old Testament, ukurasa wa 659, na Lexicon in Veteris Testamenti Libros, ukurasa wa 627. Tafsiri za mingi za Biblia zinatafsiri maneno neʹphesh na psy·kheʹ mu njia tofauti-tofauti kulingana na jambo yenye kuzungumuziwa. Kwa mufano, zinatumia maneno sawa vile “nafsi,” “uzima,” “mutu,” “kiumbe,” ao “mwili.”