Ona video zinazopatikana

Mungu Alitumia Mageuzi ili Kuumba Vitu Mbalimbali?

Mungu Alitumia Mageuzi ili Kuumba Vitu Mbalimbali?

Jibu ya Biblia

 Hapana. Biblia inasema wazi-wazi kama Mungu aliumba wanadamu na “aina” mbalimbali za wanyama na mimea. * (Mwanzo 1:12, 21, 25, 27; Ufunuo 4:11) Inasema kama wanadamu wote ni wazao wa Adamu na Eva, wazazi wetu wa kwanza. (Mwanzo 3:20; 4:1) Biblia haiunge mukono mawazo yenye kuonyesha kama Mungu alitumia mageuzi juu ya kuumba viumbe mbalimbali. Lakini, Biblia haipinge mawazo ya watu wenye kujifunza sayansi yenye kuonyesha kama mabadiliko inaweza kutokea mu aina mbalimbali za viumbe.

 Mungu alitumia mageuzi?

 Wale wenye wanaamini kama Mungu alitumia mageuzi juu ya kuumba viumbe mbalimbali wako na mawazo tofauti-tofauti juu ya namna alifanya vile. Kulingana na Encyclopædia Britannica, wamoja wao wanaamini kama “uchaguzi wa kiasili” * uko kati ya njia zenye Mungu anatumia juu ya kuongoza ulimwengu.”

 Wale wenye wanaamini kama Mungu alitumia mageuzi juu ya kuumba viumbe mbalimbali wanasemaka pia kama:

  •   Viumbe vyote vilitokana na kiumbe moja yenye iliishi zamani sana.

  •   Aina moja ya kiumbe inaweza kutokeza aina ingine ya kiumbe yenye iko tofauti kabisa.

  •   Kwa njia fulani, Mungu njo anafanya ile mambo yote ikuwe vile.

 Biblia inaunga mukono mageuzi?

 Wazo yenye kuonyesha kama Mungu alitumia mageuzi juu ya kuumba viumbe mbalimbali inatafuta kuonyesha kama habari ya uumbaji yenye kuwa mu kitabu ya Mwanzo haiko ya kweli kabisa-kabisa. Lakini, Yesu alionyesha kama habari yenye kuwa mu kitabu ya Mwanzo ni ya kweli kabisa. (Mwanzo 1:26, 27; 2:18-24; Matayo 19:4-6) Biblia inasema kama mbele Yesu akuye ku dunia, alikuwaka anaishi mbinguni pamoja na Mungu na alimusaidiaka kuumba “vitu vyote.” (Yohana 1:3) Kwa hiyo, Biblia haiunge mukono wazo yenye kuonyesha kama Mungu alitumia mageuzi juu ya kuumba viumbe mbalimbali.

 Tuseme nini kuhusu uwezo wa mimea na wanyama wa kubadilika?

 Biblia haiseme ni kwa kadiri gani mabadiliko inaweza kutokea mu aina fulani ya kiumbe. Na haipinge wazo yenye kuonyesha kama aina mbalimbali za mimea na wanyama zenye Mungu aliumba zinaweza kubadilika-badilika kadiri ziko zinazalana na kujipatanisha na fasi ya mupya. Hata kama watu fulani wanaona kama ile ni aina fulani ya mageuzi, haitokezake kiumbe fulani ya mupya.

^ Biblia inatumia neno “aina,” yenye iko na maana pana kuliko neno “espese” yenye watu wenye kujifunza sayansi wanatumiaka. Mara mingi, wakati watu wenye kujifunza mambo ya sayansi wanasema mageuzi imetokeza espese ya mupya ya kiumbe fulani, haikuwake vile. Inakuwaka tu mabadiliko yenye inatokea mu aina ileile ya kiumbe. Ni mu ileile maana njo neno aina inatumiwa mu kitabu ya Mwanzo.

^ Uchaguzi wa kiasili ni wazo yenye kuonyesha kama mumea ao munyama anaendelea kuishi kama iko na nguvu ao anakufa kama hana nguvu kulingana na vile iko anajipatanisha na hali ya kwenye anaishi.