Ona video zinazopatikana

Ni Lazima Kabisa Kuwa mu Dini Fulani?

Ni Lazima Kabisa Kuwa mu Dini Fulani?

Jibu ya Biblia

 Ndiyo. Mungu anapenda watu wakutane juu ya kumuabudu. Biblia inasema hivi: “Tufikiriane ili kutiana moyo katika upendo na matendo ya muzuri, bila kuacha kukutana pamoja.”​—Waebrania 10:24, 25, maelezo ya chini.

 Yesu alionyesha kama wanafunzi wake wangefanyiza kikundi yenye kupangwa muzuri wakati aliwaambia hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.” (Yohana 13:35) Juu ya kuonyesha ule upendo, wanafunzi wa Yesu walipaswa kukutana pamoya na waamini wenzao. Walipaswa kupangwa mu makutaniko na kukutana pamoya kwa ukawaida juu ya kumuabudu Mungu. (1 Wakorinto 16:19) Na wote, mu dunia yote, wangefanyiza familia moya ya Kikristo.​—1 Petro 2:17.

Zaidi ya kuwa mu dini fulani, mutu anapaswa kufanya nini ingine?

 Biblia inasema kama watu wanapaswa kukutana pamoya juu ya kumuabudu Mungu. Lakini haiseme kama mutu anakubaliwa na Mungu juu tu iko mu dini fulani. Juu mutu akubaliwe na Mungu, dini yake inapaswa kumusaidia atumikishe kanuni za Mungu mu maisha yake ya kila siku. Kwa mufano, Biblia inasema hivi: “Dini yenye kuwa safi na yenye haina uchafu kwa maoni ya Mungu wetu na Baba ni hii: kuhangaikia mayatima na wajane katika taabu yao, na kuendelea kubakia bila doa kutokana na ulimwengu.”​—Yakobo 1:27, maelezo ya chini.