Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Wanaheshimu Dini Nyingine?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanaheshimu Dini Nyingine?

 Tunatii shauri la Biblia kwamba ‘tuwaheshimu watu wote’—haidhuru wana imani gani ya kidini. (1 Petro 2:17, Biblia Habari Njema) Kwa mfano, katika nchi fulani kuna mamia ya maelfu ya Mashahidi wa Yehova. Hata hivyo, hatujaribu kuwashinikiza wanasiasa au wabunge wazuie au kupiga marufuku kazi ya vikundi vingine vya kidini. Wala hatujaribu kufanya kampeni ili sheria zitungwe zinazowalazimisha watu katika jamii wafuate imani yetu ya kidini na ya kiadili. Badala yake, tunaheshimu haki za wengine, kama vile tu tungependa wao waheshimu haki zetu.—Mathayo 7:12.