Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Hufanya Kazi ya Umishonari?

Je, Mashahidi wa Yehova Hufanya Kazi ya Umishonari?

 Ndiyo. Mahali popote tulipo, sisi Mashahidi wa Yehova hujitahidi kuwa na roho ya umishonari kwa kuwahubiria watu wote tunaokutana nao.​—Mathayo 28:19, 20.

 Mbali na hilo, Mashahidi fulani huhamia kwa kipindi kifupi au kirefu kwenye maeneo fulani nchini mwao yenye watu wengi ambao hawajasikia habari njema ya Biblia. Mashahidi wengine wamehamia nchi nyingine ili wafanye mengi zaidi katika kazi ya kuhubiri. Wanafurahia kushiriki kutimiza unabii huu ambao Yesu alitoa: “Mtakuwa mashahidi wangu . . . mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”​—Matendo 1:8.

 Katika mwaka wa 1943, tulianzisha shule ambayo ingewapa mazoezi ya pekee baadhi ya wamishonari wetu. Tangu wakati huo, zaidi ya Mashahidi 8,000 wamehudhuria shule hiyo ambayo inajulikana kama Shule ya Gileadi (Watchtower Bible School of Gilead).