Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 130

Uwe Mwenye Kusamehe

Uwe Mwenye Kusamehe

(Zaburi 86:5)

  1. 1. Kwa upendo Mungu,

    Kapanga Mwana afe.

    Dhambi ziweze kufutwa,

    Kifo kiondolewe.

    Tukitubu kweli kweli,

    Tunaweza kumwomba,

    Kwa msingi wa fidia,

    Aliyotoa Kristo.

  2. 2. Twapata rehema,

    Tukimwiga Yehova.

    Tukisamehe wengine,

    Kwa upendo, huruma.

    Tukiepuka kinyongo,

    Tukivumiliana;

    Tukiwaheshimu ndugu,

    Tukiwa na upendo.

  3. 3. Sote tunapaswa,

    Kuonyesha rehema.

    Itaondoa kinyongo,

    Na uchungu wa chuki.

    Tukitenda kama Mungu,

    Apendaye zaidi,

    Tutasamehe kikweli;

    Na kumwiga Yehova.