Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Comstock Images/Stockbyte via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Utachagua Kiongozi Yupi?​—Biblia Inasema Nini?

Utachagua Kiongozi Yupi?​—Biblia Inasema Nini?

 Katika majuma machache yajayo, kutakuwa na uchaguzi katika nchi kadhaa ulimwenguni. Watu wanafanya maamuzi muhimu kuhusu viongozi ambao watachagua.

 Biblia inasema nini?

Uwezo wa viongozi wanadamu una mipaka

 Biblia inataja upungufu ambao viongozi wote wanadamu wanao.

  •   “Msiwatumaini wakuu wala mwanadamu, ambaye hawezi kuleta wokovu. Pumzi yake hutoka, naye hurudi ardhini; siku hiyohiyo mawazo yake hupotea.”​—Zaburi 146:3, 4, maelezo ya chini.

 Hata viongozi wenye uwezo mkubwa zaidi hatimaye watakufa. Isitoshe, hawawezi kuhakikisha kwamba kazi zao nzuri zitaendelezwa na wale watakaokuja baada yao.​—Mhubiri 2:18, 19.

 Ukweli ni kwamba Biblia inasema wanadamu hawakupaswa kujitawala wenyewe.

  •   “Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.”​—Yeremia 10:23.

 Je, kuna yeyote anayeweza kuwa kiongozi mzuri leo?

Kiongozi aliyechaguliwa na Mungu

 Biblia inaeleza kwamba Mungu amemweka rasmi kiongozi mwenye uwezo bora na anayetegemeka kabisa: Yesu Kristo. (Zaburi 2:6) Yesu ndiye Mfalme wa Ufalme wa Mungu, serikali inayotawala kutoka mbinguni.​—Mathayo 6:10.

 Je, utaukubali uongozi wa Yesu? Biblia inaonyesha umuhimu wa uchaguzi huo:

  •   “Mheshimuni mwana [Yesu Kristo], la sivyo Mungu atawaka hasira nanyi mtaangamia kutoka njiani, kwa maana hasira Yake huwaka upesi. Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia Yeye.”​—Zaburi 2:12.

 Sasa ndio wakati wa kufanya uamuzi wako. Unabii wa Biblia unafunua kwamba Yesu alianza kutawala katika mwaka wa 1914 na kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utachukua mahali pa serikali zote za wanadamu.​—Danieli 2:44.

 Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu jinsi unavyoweza kuunga mkono uongozi wa Yesu, soma makala yenye kichwa “Amua Kuunga Mkono Ufalme wa Mungu!