Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Unapohisi Umechoshwa na Maisha

Unapohisi Umechoshwa na Maisha

HALI zinapokuwa shwari, maisha huwa mazuri sana. Lakini nyakati fulani, matatizo yanaweza kufanya tuhisi tumechoshwa na maisha.

Kwa mfano, Sally, * anayeishi Marekani, alisema hivi baada ya kimbunga kuharibu karibu kila kitu alichokuwa nacho: “Sikuwa na nguvu za kuendelea kupambana. Mara kwa mara nilihisi nikiwa karibu kabisa kukata tamaa.”

Au namna gani ukifiwa na mtu unayempenda? Janice, anayeishi Australia, anasema: “Baada ya kufiwa na wanangu wote wawili, nilipoteza kabisa mwelekeo wa maisha, hivyo ilibidi nianze kujikusanya upya. Nilimsihi Mungu na kumwambia: ‘Nimechoka! Tafadhali niache tu nipumzike. Sitaki kuamka tena.’”

Kwa upande mwingine, Daniel alichanganyikiwa sana mke wake alipofanya uzinzi. Anasema: “Mke wangu aliponiambia amefanya uzinzi, nilihisi kama nimechomwa kisu moyoni. Nilihisi maumivu makali yakinichoma tena na tena—na hali hiyo iliendelea kwa miezi kadhaa.”

Katika toleo hili la Mnara wa Mlinzi tutachunguza sababu za kutokata tamaa hata

Kwanza, tuzungumzie jinsi tunavyoweza kuvumilia tunapokumbwa na janga la asili.

^ Baadhi ya majina katika makala za toleo hili yamebadilishwa.