Hamia kwenye habari

Je, Wasomi Wanaamini Kuwa Yesu Aliwahi Kuwapo?

Je, Wasomi Wanaamini Kuwa Yesu Aliwahi Kuwapo?

 Wasomi wana msingi imara wa kuamini kwamba Yesu aliwahi kuishi. Kuhusu marejeo ya Yesu na Wakristo wa mapema yaliyofanywa na wanahistoria wa karne ya kwanza na ya pili, kitabu Encyclopædia Britannica, Toleo la 2002, kinasema hivi: “Masimulizi hayo mbalimbali yanathibitisha kwamba zamani za kale hata wapinzani wa Ukristo hawakutilia shaka kwamba Yesu alikuwa mtu halisi. Jambo hilo lilibishaniwa kwa mara ya kwanza na bila sababu nzuri mwishoni mwa karne ya 18, katika karne ya 19, na mwanzoni mwa karne ya 20.”

 Mwaka wa 2006, kitabu Jesus and Archaeology kilisema: “Hakuna msomi anayejulikana leo anayetilia shaka kwamba Myahudi aliyeitwa Yesu mwana wa Yosefu aliwahi kuishi; wengi sasa wanakubali wenyewe kwamba tunajua mambo mengi kuhusu matendo na mafundisho yake ya msingi.”

 Biblia inamtaja Yesu kuwa mtu halisi. Inatoa majina ya mababu zake na watu wake wa ukoo wa karibu. (Mathayo 1:1; 13:55) Pia, inatoa majina ya watawala maarufu walioishi wakati wa Yesu. (Luka 3:1, 2) Mambo hayo yote yanawapa nafasi watafiti wachunguze usahihi wa masimulizi ya Biblia.