Hamia kwenye habari

Wenzi wa ndoa ambao ni Mashahidi wakifurahia mikutano ya kutaniko lao kupitia njia ya video kwenye mtandao. Kwa mara ya kwanza, wengi wataadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana kwa njia hii

APRILI 3, 2020
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Mwadhimisho wa Pekee wa Kifo cha Kristo

Makutaniko Mengi Yatafanya Ukumbusho Kupitia Mtandao kwa Sababu ya Mlipuko wa Ugonjwa wa Virusi vya Corona

Mwadhimisho wa Pekee wa Kifo cha Kristo

Mamilioni ya Mashahidi na watu wanaopendezwa watakutana pamoja Jumanne, Aprili 7, 2020, ili kuhudhuria mwadhimisho wa Ukumbusho wa Kifo cha Yesu ambao ni mwadhimisho muhimu kuliko yote, unaofanywa mara moja kwa mwaka. Hata hivyo, mwaka huu, kwa sababu ya mlipuko wa virusi vya corona, mwadhimisho huu utakuwa wa kipekee sana. Watu wengi ulimwenguni pote wataunganishwa kupitia mtandao.

Kwa sababu ya mlipuko wa virusi vya corona, wenye mamlaka katika nchi nyingi wamezuia vikusanyiko vya watu wengi. Hivyo, makutaniko mengi duniani pote yamekuwa yakitumia mtandao ili kufanya mikutano yao ya kila juma. Makutaniko hayo yatatumia njia hiyo pia ili kuadhimisha Ukumbusho. Ili watu wote wanufaike, programu iliyorekodiwa itawekwa kwenye tovuti ya jw.org.

Zaidi ya watu milioni 20 walihudhuria ukumbusho mwaka uliopita. Inatarajiwa kwamba mamilioni ya watu watahudhuria Ukumbusho kwa kuunganishwa kwa njia ya video kupitia mtandao, simu, au kwa kutazama video iliyorekodiwa kwenye jw.org.

Katika nchi nyingi, ugonjwa huo unaendelea kuenea na ni hatari kwa watu wengi. Ili kuwalinda ndugu zetu, sisi sote tunahitaji kuendelea kutii kikamili miongozo inayotolewa na wenye mamlaka, mpaka hatari itakapokwisha. Lakini tuna uhakika kwamba Yehova atatusaidia, na tumeazimia kufuata amri ya Yesu inayosema “endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.”—Luka 22:19.