Hamia kwenye habari

AGOSTI 18, 2020
MSUMBIJI

Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Yatolewa katika Lugha ya Changana na Macua

Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo Yatolewa katika Lugha ya Changana na Macua

Mwisho juma wa Agosti 15 na 16, 2020, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitolewa katika mfumo wa kielektroni katika lugha ya Changana na Macua kwa wahubiri nchini Msumbiji. Wahubiri zaidi ya 8,000 wanazungumza lugha ya Changana na zaidi ya 1,700 wanazungumza lugha ya Macua.

Ndugu David Amorim, mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Msumbiji, alitoa Biblia hizo kupitia programu iliyorekodiwa mapema, na kisha wahubiri wakaitazama baadaye. Kwa kuongezea, ndugu zetu walipata ruhusa ya kurusha programu hiyo katika kituo cha televisheni pamoja na vituo vya redio zaidi ya 30.

Lugha ya Changana huzungumzwa na watu milioni 1.9 hivi wanaoishi katika mikoa miwili iliyo kusini kabisa mwa Msumbiji. Lugha hiyo inafanana na Kitsonga, inayozungumzwa na watu katika nchi jirani ya Afrika Kusini.

Eneo la watu wa Macua linapatikana katika mikoa ya kaskazini mwa Msumbiji. Lugha ya Macua huzungumzwa na watu milioni 5.8 na ni lugha ya kienyeji inayozungumzwa zaidi nchini Msumbiji.

Kwa miaka mingi, wahubiri wanaozungumza lugha hizo walikabili changamoto nyingi sana ili kupata Biblia. Biblia ziliuzwa kwa bei ghali, na katika visa fulani, maduka yaliyouza Biblia yalikataa kuwauzia Mashahidi wa Yehova. Mtafsiri mmoja anakumbuka hivi: “Nimejionea makutaniko yaliyokuwa na Biblia moja iliyotunzwa katika Jumba la Ufalme ili itumiwe na wasemaji na wale waliokuwa na migawo katikati ya juma.”

Tunashangilia na ndugu na dada zetu waliopokea Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika lugha ya Changana na Macua. Tunajua kwamba Biblia hizo zitasaidia watu wengi kupata “ujuzi sahihi wa kweli.” 1 Timotheo 2:3, 4.