Ona video zinazopatikana

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

“Nilikuwa Napenda Sana Michezo ya Kupigana”

“Nilikuwa Napenda Sana Michezo ya Kupigana”
  • Alizaliwa: 1962

  • Inchi: Amerika

  • Historia: Alipenda sana michezo ya kupigana

MAISHA YANGU YA ZAMANI

 Mwenzangu mwenye nilikuwa nafanya naye mazoezi aliumizwa mubaya sana kuliko vile nilitazamia. Nilimupiga muguu mu pua bila kutazamia. Nilijisikia kuwa mwenye hatia na kuanza kujiuliza kama nilipaswa kabisa kuendelea tena na michezo ya kupigana. Juu ya nini kosa yenye nilifanya ilinisumbua na kufanya nijiulize kama nilipaswa kabisa kuendelea na michezo ya kupigana, yenye nilipenda sana kwa miaka mingi? Muache kwanza niwafasirie namna nilianzaka michezo ya kupigana.

 Nilikomalia karibu na Buffalo, katika Inchi ya Amerika, mu New York, mu familia yenye kuwa na amani na yenye ilikuwa mu kanisa ya Wakatoliki. Nilisoma ku masomo ya Wakatoliki na nilikuwa nasaidia padri wakati wa ibada. Wazazi wetu walipenda miye na dada yangu tukuwe na maisha ya muzuri. Kwa hiyo, kama ningeweza masomo na alama ya mingi wangeniruhusu nikuwe naenda kucheza kisha kutoka ku masomo ao nitumike ma saa kidogo. Ile ilinifanya nianze kujiwekea mipaka fulani na ningali mutoto.

 Wakati nilikuwa na miaka 17, nilianza kujifunza michezo ya kupigana. Kwa miaka mingi, nilipata mazoezi saa tatu kwa siku na nilifanya vile siku sita kwa juma. Kila juma, nilikuwa napitisha pia saa za mingi nikijikumbusha namna mbalimbali ya kupigana yenye tulijifunza na niliangalia video zenye kuonyesha namna ningejua muzuri michezo ya kupigana. Nilifurahia kujizoeza na macho yangu iko yenye kufungwa na nguo fulani, hata wakati nilijizoeza kwa kutumia mipanga. Nilikuwa na uwezo wa kuvunja mbao ao litofali kwa kutumia mukono moja. Nilijua kucheza muzuri sana ile muchezo na nilipata ushindi mingi wakati wa mashindano. Michezo ya kupigana ilifikia kuwa kitu ya maana sana mu maisha yangu.

 Niliwaza kama nilikuwa nimeweza mu maisha. Nilipata diplome ku univesité na alama za mingi. Nilikuwa ingénieur wa mambo ya ordinatere katika kompani fulani yenye kujulikana. Nilipata faida mingi mu ile kompani, nilikuwa na nyumba yangu na nilikuwa na rafiki wa kimapenzi. Maisha yangu ilionekana kuwa ya muzuri sana, lakini nilikuwa na maulizo ya maana sana kuhusu maisha.

NAMNA BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU

 Juu nipate majibu ya maulizo yangu, nilianza kwenda ku kanisa mara mbili kwa juma na nilikuwa nasali Mungu anisaidie. Kisha, siku moja mazungumuzo yenye nilikuwa nayo na rafiki yangu ilibadilisha maisha yangu. Niliuliza hivi: “Ulishaka jiuliza kusudi ya maisha ni nini?”, Nikaongezea hivi: “Kuko magumu mingi sana na kuko ukosefu wa haki mingi!” Aliniambia kama naye aliulizaka maulizo ya vile na alipataka majibu ya muzuri sana mu Biblia. Alinipatia kitabu yenye kichwa Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. * Alisema kama alikuwa anajifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Ku mwanzo, nilikuwa na mashaka juu niliwaza kama nilipaswa kusoma tu kichapo ya dini yangu hapana ya dini ingine. Lakini, juu nilipenda kupata majibu ya maulizo yangu ile ilinichochea nione kama mambo yenye Mashahidi walifundisha ilikuwa kweli ao hapana.

 Nilishangaa kujua mambo yenye Biblia inafundisha kabisa. Nilijifunza kama kusudi ya Mungu ilikuwa wanadamu waishi milele katika paradiso ku dunia na ile kusudi haijabadilika. (Mwa. 1:28) Ilinishangaza kuona jina ya Mungu, Yehova, mu Biblia yangu ya King James version na nikafikia kujua kama nilikuwa nasali kuhusu ile jina wakati nilikuwa narudilia-rudilia Sala ya Bwana. (Zb. 83:18; Mt. 6:9) Pia, nilifikia kuelewa juu ya nini Mungu anaacha watu wateseke kwa wakati fulani. Mambo yote yenye nilijifunza ilikuwa ya muzuri kabisa! Nilifurahi sana.

 Sitasahau hata kidogo namna nilijisikia wakati nilianza kukusanyika ku mikutano ya Mashahidi wa Yehova. Kila mutu alinikaribisha muzuri na alipenda kujua jina yangu. Wakati nilikusanyika kwa mara ya kwanza, hotuba ya pekee ya watu wote yenye ilitolewa ilizungumuzia sala zenye Mungu anakubali. Nilipenda sana kichwa ya ile hotuba, juu nilikuwa nasali Mungu anisaidie. Kisha nilienda ku Ukumbusho ya kifo ya Yesu. Ku ile mikutano, nilishangaa kuona hata watoto kidogo wanafuata usomaji wa maandiko katika Biblia. Ku mwanzo, sikukuwa najua namna ya kupata maandiko, lakini Mashahidi walinisaidia sana na walinifundisha namna ya kutumikisha Biblia.

 Kisha kukusanyika mara mingi, nilianza kupenda kabisa mafundisho ya muzuri sana yenye Mashahidi walifundisha. Nilijifunza mambo mingi ku kila mukutano, na kila mara nilikuwa najisikia mwenye kutiwa moyo na mwenye kutulia. Kisha Mashahidi waliniambia nikuwe na funzo ya Biblia ya kipekee.

 Mambo yenye niliona kati ya Mashahidi wa Yehova ilikuwa kabisa tofauti na mambo yenye nilizoea kuona mu kanisa yetu. Niliona vile Mashahidi walikuwa na umoja na vile ni kikundi ya watu wazuri wenye wanafanya yao yote ili kumupendeza Mungu. Nilikomala na niko hakika kama Mashahidi wa Yehova walionyesha sifa yenye kuwatambulisha kama ni wa wakristo wa kweli, ni kusema, walionyesha upendo kati yao.​—Yoh. 13:35.

 Kadiri nilijifunza Biblia ni vile nilifanya mabadiliko ili kuishi kulingana na kanuni za Biblia. Lakini, nilijisikia sawa vile singeweza kuacha michezo ya kupigana. Nilikuwa napenda mazoezi na mashindano. Wakati niliambia Shahidi mwenye nilikuwa najifunza naye Biblia ile jambo, kwa upole alinihakikishia hivi, “Endelea tu kujifunza na najua utakamata uamuzi wa muzuri.” Ile ilikuwa kabisa maneno yenye nilipenda kusikia. Kadiri niliendelea kujifunza ni vile nilipenda kumupendeza Yehova.

 Jambo ingine kunihusu ni ya ile hali yenye ilitokea yenye nilitaja ku mwanzo, wakati nilipiga mwenzangu mwenye tulikuwa nafanya naye mazoezi muguu mu pua bila kutazamia. Ile ilinifanya nifikiri sana kama ningekuwa kabisa mwanafunzi wa Kristo mwenye kufanya amani ikiwa naendelea kucheza michezo ya kupigana. Nilijifunza kama Isaya 2:3, 4 ilitabiri kuwa wale wenye wanafuata miongozo ya Yehova “hawatajifunza vita tena.” Na Yesu alifundisha watu kama hawapaswe kutenda kwa jeuri hata kama wanatendewa bila haki. (Mt. 26:52) Njo maana niliacha kucheza ile michezo yenye nilikuwa napenda sana.

 Kisha pale, nilifuata shauri ya Biblia ya ‘kujizoeza ukiwa na kusudi la ushikamanifu kwa Mungu.’ (1 Ti. 4:7) Wakati na nguvu yote yenye nilikuwa natoa mu michezo ya kupigana niliitumia sasa ili kumukaribia Mungu na kumutumikia. Rafiki wangu wa kimapenzi hakukubaliana na mambo yenye nilikuwa najifunza mu Biblia njo maana tuliachana. Nilibatizwa tarehe 24 mwezi wa 1, 1987. Kisha masiku kidogo, nilianza kazi ya utumishi wa wakati wote, nilitumia wakati yangu ili kufundisha wengine Biblia. Tangu ile wakati niliendelea mu utumishi wa wakati wote na wakati fulani nilitumika ku makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova mu Inchi ya Amerika ku New York.

NAMNA NILIPATA FAIDA

 Sasa vile najua kweli kuhusu Mungu, nimepata mambo yenye nilikuwa nakosa mu maisha yangu. Sijisikie tena kama sina kitu. Lakini niko na kusudi ya muzuri mu maisha, tumaini ya kweli juu ya wakati wenye kuja, na najisikia kuwa mwenye furaha kabisa. Naendelea kujizoeza kikawaida, lakini mazoezi ya kimwili haiko njo tena jambo ya maana sana kwangu. Jambo ya maana sana mu maisha yangu ni kumutumikia Yehova Mungu.

 Wakati nilikuwa najifunza michezo ya kupigana, kila mara nilikuwa muangalifu kuhusu watu wenye kunizunguuka juu kila mara nilikuwa nawaza namna naweza kujitetea kama mutu ananichokoza. Leo, naendelea tu kuwa muangalifu kuhusu watu wenye kunizunguuka lakini nafanya vile juu ya sababu yenye kuwa tofauti na ile ya zamani, ni kusema, kusaidia watu. Biblia imenisaidia nifikie kuwa mukarimu na bwana muzuri kwa bibi yangu Brenda.

 Nilikuwa napenda sana michezo ya kupigana mu maisha yangu. Lakini, niliibadilisha na jambo fulani ya muzuri sana. Biblia inasema muzuri kabisa kuhusu ile hivi: “Mazoezi ya mwili ni yenye faida kidogo, lakini ushikamanifu kwa Mungu uko na faida katika mambo yote, kwa maana uko na ahadi ya uzima wa sasa na ya ule wenye utakuja.”​—1 Ti. 4:8.

^ Ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova lakini kwa sasa haichapishwe tena.