Ona video zinazopatikana

Ndoa ya Mashahidi wa Yehova Inakuwaka Namna Gani?

Ndoa ya Mashahidi wa Yehova Inakuwaka Namna Gani?

 Kwa kawaida, ndoa ya Mashahidi wa Yehova haikuwake na mambo mingi na inafanyikaka kwa heshima. Kunakuwaka hotuba yenye inategemea Biblia. Kisha hotuba, watu wanaweza kukutana ili kula pamoya. a Yesu aliendaka pia ku karamu ya ndoa mu muji wa Kana ku mwanzo-mwanzo wa utumishi wake.​—Yohana 2:1-11.

 Mambo inakuwaka namna gani ku sherehe ya ndoa?

 Hotuba ya ndoa, ni sehemu ya maana sana mu sherehe ya ndoa. Inakamataka dakika 30 hivi na inatolewaka na mutumishi wa kutaniko wa Mashahidi wa Yehova. Hotuba yenye kuchangamuka na yenye kutia moyo inaonyesha namna Biblia inaweza kusaidia bibi na bwana kuwa na ndoa yenye kudumu, yenye upendo, na yenye furaha.​—Waefeso 5:33.

 Mu inchi za mingi, serikali inaruhusu watumishi wa kidini wa Mashahidi wa Yehova waunganishe bibi na bwana katika kifungo ya ndoa. Mu ile hali, ku mwisho wa hotuba, bibi na bwana wanafanya naziri. Wanaweza pia kuvalishana pete. Kisha, ule mutumishi wa kidini wa Mashahidi wa Yehova anawatangaza kuwa bibi na bwana.

 Mu inchi zingine, sheria inaomba bibi na bwana kuoana ku biro ya serikali. Bibi na bwana wanafanya vile mbele hotuba ya ndoa itolewe. Kama bibi na bwana hawakufanya naziri ya ndoa ku biro ya serikali, wanaweza kufanya vile ku mwisho wa hotuba. Kama walifanya naziri ya ndoa ku biro ya serikali, wanaweza kuamua kuirudilia, kwa kuisema mu wakati yenye ilishapita juu ya kuonyesha kama walikuwa tayari walishafanya naziri yao. Hotuba inamalizika na sala ya kumuomba Mungu abariki bibi na bwana wenye wametoka kuoana.

 Ndoa ya Mashahidi wa Yehova inafanyiwaka wapi?

 Mashahidi wa Yehova wengi wanachaguaka kufanya sherehe yao ya ndoa ku Jumba ya Ufalme kama iko tayari. b Kama bibi na bwana wanapanga kufanya karamu kisha hotuba, wanatafutaka fasi ingine juu ya kufanya vile.

 Nani njo anaweza kuenda ku ndoa?

 Kama ndoa inafanyiwa ku Jumba ya Ufalme, kwa kawaida kila mutu anaweza kuenda, ni kusema, Mashahidi na wenye hawako Mashahidi. Kama bibi na bwana wanapenda kufanya karamu, wataamua ni nani njo wataalika.

 Watu wanapaswa kuvala namna gani?

 Wakati ndoa zinafanywa ku Jumba ya Ufalme, watu hawaombwe kuvala mu njia fulani, lakini Mashahidi wa Yehova wanajikaza kufuata kanuni za Biblia ili kuvala kwa kiasi na kwa heshima. Ni muzuri kama kila mutu anafuata zile kanuni ku ndoa. (1 Timoteo 2:9) Na zile kanuni zinapaswa pia kufuatwa fasi kwenye bibi na bwana wanapenda kufanyia karamu.

 Waalikwa wanaweza kuleta zawadi?

 Biblia inatutia moyo kutoa kwa kupenda. (Zaburi 37:21) Mashahidi wa Yehova wanafurahiaka kutoa na kupokea zawadi za ndoa. (Luka 6:38) Lakini, wanaepuka kuomba zawadi na kutangaza majina ya wale wenye walitoa zawadi. (Matayo 6:3, 4; 2 Wakorinto 9:7; 1 Petro 3:8) Kufanya vile ni kupinga mambo yenye Biblia inasema, na ile inaweza kuletea haya waalikwa.

 Waalikwa wanagonganishaka virauli kwa ajili ya wale wenye kuoana?

 Hapana. Mashahidi wa Yehova hawagonganishake virauli juu kugonganisha virauli ilianza mu desturi za dini ya uongo. c Mashahidi wa Yehova wanatakia bibi na bwana mambo ya muzuri mu njia zingine.

 Waalikwa wanatupiaka wale wenye kuoana muchele ao karatasi za kidogo-kidogo?

 Hapana. Mu maeneo fulani, watu wanatupiaka bibi na bwana wenye wametoka kuoana muchele ao karatasi za kidogo-kidogo, ao kitu ingine yenye inafanana na ile. Wanaamini kama ile italetea bibi na bwana bahati, furaha, na maisha ya murefu. Mashahidi wa Yehova wanaepuka kufanya mambo yenye iko na uhusiano na ushirikina. Mashahidi wa Yehova hawatakie wengine bahati juu ile inapingana kabisa na mambo yenye Biblia inasema.​—Isaya 65:11.

 Kunakuwaka chakula na kinywaji?

 Sherehe ya ndoa yenye inafanywa ku Jumba ya Ufalme haikuwake na chakula ao kinywaji. Bibi na bwana fulani wanaamua kufanya karamu kisha hotuba ya ndoa fasi kwenye wanaweza kukula na kunywa. (Muhubiri 9:7) Kama wanaamua kupatia watu pombe, wanaepuka kutoa pombe mingi sana juu waalikwa wasilewe, na wanapatia pombe wale tu wenye kisheria wako na miaka ya kunywa pombe.​—Luka 21:34; Waroma 13:1, 13.

 Kunakuwaka muziki na dansi?

 Kama bibi na bwana wanapenda kufanya karamu, wanaweza kuamua kutia miziki na dansi. (Muhubiri 3:4) Watachagua miziki yenye wanapenda na yenye watu wa desturi yao wanapenda, lakini watahakikisha kama ni miziki yenye kufaa. Kwa kawaida sherehe ya ndoa yenye inafanyika ku Jumba ya Ufalme inakuwaka na nyimbo zenye zinategemea Maandiko.

 Mashahidi wa Yehova wanakumbukaka siku yao ya ndoa?

 Juu kanuni za Biblia hazikubali wala kukataza kukumbuka siku ya ndoa, bibi na bwana Mashahidi watajiamulia ikiwa watakukumbuka siku yao ya ndoa ao hapana. Kama wanaamua kuikumbuka, wanaweza kufanya vile wao wenyewe ao pamoya na marafiki wao ao tena pamoya na watu wa familia yao.

a Kila eneo iko na desturi na sheria zake kuhusu ndoa.

b Hawalipake makuta yoyote ule mutumishi wa kutoa hotuba, na hakuna makuta yoyote yenye inaombwa ili kutumia Jumba ya Ufalme.

c Ili kujua mambo mingi juu ya kugonganisha virauli, ona habari “Maulizo ya Wasomaji Wetu” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 2, 2007.