WIMBO 106
Tukuwe na Upendo
-
1. Yehova utusaidie
Kuwa na sifa kama zako.
Zaidi ya yote upendo
Wenye unatoka mu moyo.
Na kama hatuna upendo,
Imani yetu ni ya bure.
Basi tuonyeshe upendo
Kwa maneno na kwa matendo.
-
2. Upendo unatusukuma
Kuwasaidia wengine,
Na kusamehe ndugu zetu;
Ni vile Yesu alisema.
Upendo unavumilia
Na unafunika makosa.
Tutavumilia magumu
Ikiwa tuko na upendo.
(Ona pia Yoh. 21:17; 1 Ko. 13:13; Gal. 6:2.)