Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NAMNA MICHANGO YAKO INATUMIWA

Kutolea Ndugu na Dada Misaada Wakati ya Coronavirus

Kutolea Ndugu na Dada Misaada Wakati ya Coronavirus

Tarehe 1, Mwezi wa 7, 2021

 Mwezi wa 3, 2020, wakati shirika ya Umoja wa Mataifa yenye inahangaikia mambo ya afya ilitangaza kama Coronavirus imeenea mu dunia yote, watu wengi hawakuwazia hata kama Coronavirus itakuwa ingali kisha mwaka moya. Ule ugonjwa ulifanya mamilioni ya watu, kutia ndani Mashahidi wa Yehova fulani, wakuwe na matatizo ya afya, mahangaiko, na kukosa makuta. Mashahidi wa Yehova walifanya mipango gani juu ya kusaidia ndugu na dada mu ile kipindi?

Musaada Kwa Wale Wenye Walikuwa mu Uhitaji

 Chini ya muongozo ya Halmashauri ya Waratibu ya Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova, zaidi ya Halmashauri za Kutoa Misaada 950 zimeanzishwa juu ya kutoa misaada mu dunia yote wakati ya Coronavirus. Ndugu na dada fulani wamesaidiwa na Halmashauri za Kutoa Misaada zenye kuwa mu eneo yao. Na wengine wamesaidiwa na serikali. Zile halmashauri zilikamata pia mipango juu ya kutoa misaada mu dunia yote.

 Kwa mufano, fikiria mambo yenye ilitokea mu Paraguay. Gazeti moya ilisema kama juu ya Coronavirus, “wakaaji wengi wa Paraguay wanakosa chakula mu nyumba zao.” Lakini, Halmashauri ya Kutoa Misaada mu Paraguay tayari imeanza kugawanya vitu vya lazima vyenye familia ya watu 4 inaweza kutumia mu juma mbili, sawa vile, chakula, vitu vya kutumia ili kusafisha nyumba, na vitu vingine kwa ajili ya usafi wa mwili. Vitu vyenye kila familia ilipewa vilikuwa na samani ya dolare 30.

 Ndugu na dada wenye walisaidia mu kazi ya kutoa misaada walifanya nini juu ya kujilinda na kulinda wengine wasiambukizwe na Coronavirus? Walivala masques, na waliepuka kukaribiana sana na watu wengine. Walichunguza pia kama kompanyi zenye zinawauzisha na kuwaletea chakula zinatumiaka madepo yenye kuwa safi, na kama ziko zinafuata maagizo juu ya kujilinda na ugonjwa. Kwa mufano, walihakikisha kama wale wote wenye watagusa vile vitu walipaswa kuvala vitu vya kuwalinda, walisafisha na kuua mikrobe mu gari zenye walitumia, na kuweka vile vitu fasi kwenye kumesafishwa na dawa ya kuua mikrobe. Ku mwisho, wale wenye walikuwa nagawia ndugu na dada vile vitu waliepuka kukaribiana sana nao.

Kutumia Michango Kwa Hekima

 Halmashauri ya Waratibu ilikubali dolare milioni 25 zitumiwe juu ya kusaidia ndugu na dada wakati ya Coronavirus. Biro za Tawi na Halmashauri za Kutoa Misaada zilitumia michango kwa uangalifu, na zilijikaza sana kununua vitu vya lazima ku bei ya muzuri. Kwa mufano, mu inchi ya Chili, ndugu wenye waliongoza kazi ya kutoa misaada walipenda kununua kilo 750 ya dengu (ao lentilles). Bei ya dengu ilikuwa imepanda mara mbili mu mwezi moya tu! Lakini, ndugu walikuwa wamekubali kuuza ile dengu ku bei ya juu. Na kisha saa mbili, mwenye kuuzisha aliwajulisha kama mutu mwingine mwenye angeuza alisema kama hatauza tena. Kwa hiyo, kuliko kuwauzisha ku ile bei ya juu yenye walisikilizana, mwenye kuuzisha aliambia ndugu kama waibebe ku bei ya zamani!

 Wakati ndugu zetu walienda kukamata ile ndegu, mwenye kuuzisha alitaka kuwakatalia. Aliwashitaki kama walikuwa na ubaguzi wakati walikuwa nagawia watu chakula, sawa vile matengenezo ingine inafanyaka. Kisha kutoa sala ya mufupi na ya kimya-kimya, ndugu yetu aliambia mwenye kuuzisha kama tayari kila kutaniko imechunguza juu ya kuona nani njo iko kabisa na lazima ya musaada. Ndugu zetu walimufasiria pia kama juu wale wenye watapewa misaada ni wa desturi mbalimbali, kila watu watapokea vitu vyenye wanazoea kutumia. Ku mwisho, walihakikishia mwenye kuuzisha kama ile makuta yote ni michango ya kuijipendea ya Mashahidi wa Yehova, na wale wote wenye wanatumika mu kazi ya kutoa misaada wanaifanya kwa kujipendea. Akashangaa sana. Kwa hiyo, mwenye kuuzisha alikubali kuwapunguzia bei. Lakini pia, siku walikuya tena kuuza, naye alitoa muchango wa kilo 400 za dengu.

“Alama ya Upendo wa Kweli”

 Lusu, mwanamuke mujane wa Liberia, anaishi na watu tano wa mu familia yake. Siku moya asubui wakati walikuwa nakula chakula ya asubui na kuchunguza andiko ya siku, mujukuu wa Lusu wa miaka saba alitambua kama hawakukuwa tena na chakula mu nyumba. Kisha akauliza hivi: “Tutakula nini?” Lusu alimuhakikishia kama alishasali juu ya ile jambo, na kama iko hakika kuwa Yehova atawapatia mambo yenye wako nayo lazima. Ileile siku wakati ilifika muchana, wazee wa kutaniko ya Lusu walimuita juu aende kukamata misaada ya chakula. Anasema hivi: “Mujukuu wangu anasema kama sasa anatambua kuwa Yehova anasikilizaka na kujibia sala, juu Yehova amejibia sala yangu.”

Picha zenye watoto wa mu Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo walichapa juu ya kushukuru ndugu na dada zao kwa ajili ya misaada ya chakula yenye walipokea

 Mu Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, mwanamuke moya alikuwa naishi karibu na familia moya ya Mashahidi. Kisha kuona Mashahidi wengine wanaletea ile familia chakula, alisema hivi: “Wakati Coronavirus itaisha, tutakuwa Mashahidi wa Yehova, juu wamehangaikia ndugu na dada zao mu hii kipindi ya nguvu sana.” Bwana yake akamuuliza hivi: “Utakuwa Shahidi wa Yehova juu tu ya saki moya ya muchele?” Akamujibia hivi: “Hapana, lakini ile saki ya muchele ni alama ya upendo wa kweli.”

 Michango yako ya kujipendea njo imefanya Mashahidi wa Yehova waweze kusaidia haraka ndugu na dada zetu mu hii kipindi ya Coronavirus. Tunakushukuru sana juu ya michango yenye umetoa kwa kutumia njia zenye kuonyeshwa ku donate.isa4310.com.