Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Rushwa Yenye Kuwa mu Serikali Itaishaka?

Rushwa Yenye Kuwa mu Serikali Itaishaka?

 Mu dunia yote, wakubwa wa serikali wanapanaka rushwa (ao, kata-midomo; ao tena, kanyaka), na ile inakuwaka na matokeo mingi ya mubaya. a Kwa mufano, mu hii kipindi ya ugonjwa wa coronavirus, inasemekana kama mu inchi za mingi wakubwa fulani wa serikali ao guvernema walijifanya kuwa matajiri na makuta yenye walipewa juu ya kupambana na ugonjwa wa coronavirus. Rushwa ya vile, ilifanya watu wengi wakose kupata matunzo yenye walikuwa nayo lazima, kwa hiyo, iliongeza mateso na hata kifo.

 Rushwa inaenea sana. David Cameron, waziri mukubwa wa zamani wa Uingereza, alisema hivi: “Rushwa iko sawa nyumba ya buibui na mainchi yote ilishakamatika ndani.”

 Hata vile, tunaweza kuwa hakika kama hivi karibuni, rushwa ya kila namna yenye kuwa mu serikali itaisha. Juu ya nini tunasema vile? Ona mambo yenye Biblia inasema kama Mungu atafanya.

Nini inafanya tukuwe hakika kama Mungu atamaliza rushwa?

 Mu Biblia, muko hii maneno ya Mungu: “Kwa maana mimi, Yehova, ninapenda haki; ninachukia unyanganyi na ukosefu wa haki.” b (Isaya 61:8) Mungu anaona wakati watu wanateseka kwa sababu wengine walitoa rushwa. (Mezali 14:31) Anaahidi hivi: “Kwa sababu wale wenye kuteswa wanakandamizwa, . . . Nitasimama ili kutenda.”​—Zaburi 12:5.

 Mungu atafanya nini? Kuliko kutengeneza serikali zenye kuwa leo, Mungu atazitosha na atatia serikali yake ya mbinguni, yenye inaitwa “Ufalme wa Mungu.” (Marko 1:14, 15; Matayo 6:10) Biblia inasema hivi: “Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme wenye . . . utaponda na kumaliza falme hizi [zingine] zote, na ufalme huo peke yake utasimama milele.” (Danieli 2:44) Kwa hiyo, kupitia ufalme wake, Mungu atamaliza rushwa yote yenye tuko naona leo.

Serikali yenye haitakuwa na rushwa

 Tunajua namna gani kama mu Ufalme wa Mungu hamutakuwa rushwa? Ona mambo yenye kufuata.

  1.  1. Mamlaka. Mamlaka ya Ufalme wa Mungu inatoka kwa Mungu Mweza-yote.​—Ufunuo 11:15.

     Juu ya nini ile ni jambo ya lazima? Juu serikali itumike inaomba makuta, na makuta inatokaka kwa wanainchi. Mara mingi, ile njo inafanya kukuwe wizi, rushwa na mambo ingine ya vile. Lakini, Ufalme wa Mungu unategemezwa na Mungu Mweza-yote, njo maana utakuwa kila siku na uwezo wa kupatia raia wake mambo yenye wako nayo lazima.​—Zaburi 145:16.

  2.  2. Kiongozi. Mungu alimuchagua Yesu kuwa Kiongozi wa Ufalme wake.​—Danieli 7:13, 14.

     Juu ya nini ile ni jambo ya lazima? Hata kiongozi muzuri zaidi anaweza kushawishiwa kufanya mambo ya mubaya. (Muhubiri 7:20) Lakini, matendo ya Yesu ilionyesha kama hakuna mutu anaweza kumuchochea afanye mambo ya mubaya. (Matayo 4:8-11) Zaidi ya ile, upendo wenye Yesu iko nao juu ya raia wa Ufalme wa Mungu, na namna anahangaikia hali ya muzuri ya watu njo inamuchochea kutenda.​—Zaburi 72:12-14.

  3.  3. Sheria. Sheria ya Ufalme wa Mungu ni kamilifu, na inaleteaka furaha wenye kuifuata.​—Zaburi 19:7, 8.

     Juu ya nini ile ni jambo ya lazima? Sheria za wanadamu ziko mingi, ni nguvu kuzifuata, na wakati fulani haziko wazi kabisa. Njo maana ile inafungulia watu mulango wa kutumia rushwa. Lakini, sheria za Mungu ziko wazi na zinatuletea faida. (Isaya 48:17, 18) Zaidi ya ile, sheria za Mungu haziguse tu matendo, lakini pia nia. (Matayo 22:37, 39) Kwa kweli, Mungu anaweza kusoma mu mioyo ya watu na anahakikisha kama sheria zake ni za muzuri.​—Yeremia 17:10.

 Tunakutia moyo ujifunze zaidi kuhusu mambo yenye Biblia inasema juu ya serikali yenye iko nakuya, serikali yenye haitakuwa na mambo ya rushwa.

a Kulingana na kitabu fulani, “rushwa” ni kutumia mubaya mamlaka juu ya kujipatia faida.

b Yehova ni jina ya pekee ya Mungu. (Zaburi 83:18) Soma habari “Yehova Ni Nani?