Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

TheCrimsonMonkey/E+ via Getty Images

Mazingira Inaharibika​—Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?

Mazingira Inaharibika​—Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?

 “Namna hali ya hewa inaharibika inahangaisha watu sana, iko na matokeo mubaya juu ya miji yetu, wanyama na mimea. Upepo mukali wenye unaendelea kuwa nguvu kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya hewa unaharibisha nyumba za watu na kazi zenye zinawasaidia kuishi. Kifukutu iko naendelea kuongezeka mu bahari na ile inaweza kufanya viumbe wengi wa mu bahari wakufe.”​—Inger Andersen, Sous-secretaire wa Katibu mukuu wa Umoja wa Mataifa na mukurugenzi mutendaji wa Mupango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa, tarehe 25 Mwezi wa 7, 2023.

 Serikali zinaweza kutumika pamoya ili kumaliza hii matatizo yenye inahusu dunia yote? Je, wataweza kabisa kumaliza ile matatizo?

 Biblia inazungumuzia serikali yenye iko na uwezo wa kutengeneza mazingira yote na ile serikali itafanya vile. Biblia inasema “Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme,” ni kusema serikali yenye itatawala dunia yote na kumaliza matatizo yote ya dunia. (Danieli 2:44) Chini ya ile serikali watu “hawatatokeza jambo lolote lenye kuumiza wala uharibifu wowote” juu ya mumoja na mwingine na juu ya dunia.​—Isaya 11:9.