Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maremagnum/Corbis Documentary via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Armagedoni Itaanzia Israeli?—Biblia Inasema Nini?

Armagedoni Itaanzia Israeli?—Biblia Inasema Nini?

 Biblia inasema kama Armagedoni haiko vita yenye itapiganwa mu eneo moya tu, lakini ni vita yenye itapiganwa mu dunia yote kati ya serikali za wanadamu na Mungu.

  •   “Maneno yenye yanaongozwa na pepo wachafu . . . yanaenda kwa wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu, ili kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote. . . . yakawakusanya pamoja mahali kwenye kunaitwa katika Kiebrania Armagedoni.”​—Ufunuo 16:14, 16.

 Neno “Armagedoni” inatokana na neno ya Kiebrania Har Meghid·dohnʹ, maana yake “Mulima wa Megido.” Megido ilikuwa muji wenye ulipatikana mu Israeli ya zamani. Njo maana watu fulani wanaamini kama Armagedoni itapiganwa mu Israeli. Lakini eneo ya Megido ao eneo yoyote ya Asia ya kati haina fasi ya kutosha kwenye kutaenea “Wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu” na majeshi yao.

 Kitabu ya Ufunuo kiliandikwa kwa njia ya “alama” ao maneno ya mufano. (Ufunuo 1:1) Armagedoni haiko eneo fulani, lakini ni hali ya mataifa ya mu dunia yote ya kujaribu kwa mara ya mwisho kupinga utawala wa Mungu.​—Ufunuo 19:11-16, 19-21.