Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Surasak Suwanmake/Moment via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Mu Dunia Yote Kipindi ya Kifukutu ya 2023 Iko na Joto Sana​—Biblia Inasema Nini?

Mu Dunia Yote Kipindi ya Kifukutu ya 2023 Iko na Joto Sana​—Biblia Inasema Nini?

 Watu wa mu dunia yote wanapambana na hali ya kifukutu ya sana na matokeo ingine ya ile hali. Ona habari zenye kufuata:

  •   “Hii mwezi wa 6 njo mwezi ya kifukutu sana mu miaka 174 tangu watu waanze kurekodi hali ya hewa.”​—National Oceanic and Atmospheric Administration, U.S. Département du commerce des États-Unis, tarehe 13 Mwezi wa 7, 2023.

  •   “Mu inchi za Italia, Espagne, Ufaransa, Alemayne na Polonye watu wanapambana na kifukutu ya juu, na inatazamiwa kwamba kifukutu ya hewa itafika mu 48°C [118°F] mu visiwa vya Sicile na Sardaigne; ile inaweza kuwa kifukutu ya juu sana kurekodiwa mu Ulaya.”​—Shirika la anga za juu la Ulaya, tarehe 13 Mwezi wa 7, 2023.

  •   “Vile dunia inaendelea kuwa na kifukutu zaidi, inatazamiwa kwamba mvua itakuwa mingi sana na ya nguvu sana yenye itafaya maji ikuwe najaa sana kweye mito mupaka inavuka mipaka yake.”​—Stefan Uhlenbrook, mukurugenzi wa hydrolojia, maji na cryosphere katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani, tarehe 13 Mwezi wa 7, 2023.

 Ripoti zenye kuongezeka kuhusu kifukutu ya sana inakuhangaisha? Ona mambo yenye Biblia inasema juu ya hii habari ya maana.

Kifukutu ya sana inatimiza unabii wa Biblia?

 Ndiyo. Kifukutu ya sana ya mu dunia yote na hali zingine za hewa zenye kuhangaisha zinapatana na mambo yenye Biblia ilitabiri juu ya wakati wetu. Kwa mufano, Yesu alitabiri kama tutuaona “mambo yenye kuogopesha.” (Luka 21:11) Juu kifukutu inaendelea kuongezeka watu wengi wameanza kuogopa juu wanawaza kama wanadamu wataharibu dunia.

Je, wakati fulani haitawezekana tena kuishi ku dunia?

 Hapana. Mungu aliumba dunia ili ikuwe makao yetu milele; hataruhusu wanadamu waiharibu. (Zaburi 115:16; Muhubiri 1:4) Hata, ameahidi “kuharibu wale wenye wanaharibu dunia.”​—Ufunuo 11:18.

 Biblia inaonyesha kama Mungu iko na uwezo wa kulinda dunia juu isiharibike na kama atafanya vile.

  •   “[Mungu] anatuliza zoruba yenye upepo mukali; Mawimbi ya bahari yananyamaza” (Zaburi 107:29). Mungu iko na uwezo juu ya nguvu za asili. Iko na uwezo wa kutengeneza mazingira yenye imeharibika yenye inafanya watu wateseke kwa sababu ya kifukutu ya sana.

  •   “Unatunza dunia, Unaifanya izae kwa wingi na kuifanya ikuwe tajiri sana.” (Zaburi 65:9) Mungu atabariki dunia na kuifanya ikuwe paradiso.

 Ili kujua mengi juu ya ahadi ya Mungu ya kutengeneza mazingira, soma habari “Ni Nani Atakayeiokoa Dunia?