Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunaweza Kabisa Kumufurahisha Mungu?

Tunaweza Kabisa Kumufurahisha Mungu?

Kuna siku umesoma juu ya watu wenye kusifiwa sana katika Biblia na kusema hivi: ‘Siwezi kuwa kama wao!’ Unaweza kuwaza hivi: ‘Mimi ninafanya makosa, siko mwenye haki, na kila mara sifanye yaliyo sawa.’

Ayubu alikuwa mwanaume ‘asiye na lawama na munyoofu.’

Ayubu 1:1

Biblia inasema kuwa Ayubu alikuwa ‘asiye na lawama [kosa] na munyoofu.’ (Ayubu 1:1) Loti aliitwa mutu ‘muadilifu [mwenye haki].’ (2 Petro 2:8) Na Biblia inasema kuwa Daudi alikuwa anafanya “yaliyokuwa sawa” machoni pa Mungu. (1 Wafalme 14:8) Lakini, tuzungumuzie kwa uangalifu maisha ya watu hao wenye kutajwa katika Biblia. Tutaona kuwa (1) walifanya makosa, (2) mifano yao inaweza kutufundisha mambo mengi, na (3) wanadamu wasiokamilika wanaweza kabisa kumufurahisha Mungu.

WALIFANYA MAKOSA

“[Mungu] alimukomboa Loti muadilifu, aliyetaabishwa sana na kule kujitia katika mwenendo mupotovu kwa watu wanaokaidi [wanaovunja] sheria.’—2 Petro 2:7

Ayubu alipata magumu mengi, na ilionekana hakustahili kupata magumu hayo. Alianza kuwa na mawazo mabaya. Aliwaza kama Mungu hahangaike ikiwa iko na imani kwake ao hapana. (Ayubu 9:20-22) Ayubu alikuwa hakika kabisa kuwa yeye ni mwenye haki, na watu wengine waliona kuwa alikuwa anajitangaza kuwa mwenye haki kuliko Mungu.—Ayubu 32:1, 2; 35:1, 2.

Loti alisita kuchukua uamuzi wenye ulionekana kuwa mudogo na wenye kuwa wazi. Alihuzunishwa sana na mwenendo mubaya wa watu wa Sodoma na Gomora. Na hata alikuwa ‘anaitesa nafsi yake yenye uadilifu [haki]’ kwa sababu ya tabia yao. (2 Petro 2:8) Mungu alisema kuwa ataharibu miji hiyo yenye matendo mabaya, na akapatia Loti nafasi ya kuokoka pamoja na familia yake. Unaweza kuwazia kuwa Loti aliyekuwa na huzuni sana ndiye angekuwa wa kwanza kuondoka. Lakini wakati huo wa hatari, Loti alikawia kuondoka. Malaika wenye walitumwa ili kumuokoa yeye na familia yake, walilazimika kuwakamata kwenye mikono, na kuwapeleka mahali salama inje ya muji.—Mwanzo 19:15, 16.

Daudi ‘alifuata [Mungu] kwa moyo wake wote kwa kufanya yaliyokuwa sawa tu machoni [pa Mungu].’—1 Wafalme 14:8

Daudi naye wakati fulani alishindwa kujizuia na akafanya uzinifu na bibi ya mwanaume mwengine. Jambo la mubaya zaidi ni kuwa alipanga bwana ya mwanamuke huyo auawe ili kujaribu kuficha zambi yake. (2 Samweli, sura ya 11) Biblia inasema kuwa jambo lenye Daudi alifanya lilikuwa ‘mbaya machoni pa Yehova.’—2 Samweli 11:27.

Ayubu, Loti, na Daudi, wote walifanya makosa, na makosa fulani yalikuwa makubwa. Lakini, kama vile tutaona, walikuwa na tamaa ya kumutumikia Mungu na kumutii kwa moyo wote. Wakati walifanya makosa, walikuwa tayari kuomba musamaha na kubadilika. Kwa hiyo, Mungu aliwakubali, na wakati Biblia inazungumuza juu yao, inaonyesha kuwa walikuwa wanaume waaminifu.

MIFANO HIYO INATUFUNDISHA NINI?

Kwa sababu sisi ni wanadamu wasiokamilika, hatuwezi kuepuka kufanya makosa. (Waroma 3:23) Lakini wakati tunafanya makosa, tunapaswa kuomba musamaha na kisha tunapaswa kufanya yetu yote ili kubadilika.

Namna gani Ayubu, Loti, na Daudi walijikaza kubadilika? Katika moyo wake, Ayubu alikuwa mutu mushikamanifu. Wakati Mungu alifikiri pamoja naye, Ayubu alibadilisha mawazo yake na akaomba musamaha juu ya mambo yenye alikuwa amesema. (Ayubu 42:6) Loti alichukia mwenendo mubaya wa watu wa Sodoma na Gomora, kama vile tu Mungu alichukia mwenendo huo. Shida ni kwamba wakati huo alikosa kutenda kwa haraka. Mwishowe, Loti alitoka katika muji huo wenye Mungu alipanga kuharibu na akaepuka hukumu ya Mungu. Alimutii Mungu kwa kuwa hakuangalia hata mambo yenye alikuwa ameacha nyuma. Hata kama Daudi alifanya kosa kubwa kwa kuvunja sheria ya Mungu, alionyesha mambo yenye yalikuwa katika moyo wake wakati alitubu kutoka moyoni, na kuomba Mungu amusamehe.—Zaburi 51.

Mungu alikubali wanaume hao, na hilo linaonyesha kama haombe wanadamu wasiokamilika wafanye mambo yenye kupita uwezo wao. Mungu ‘anajua vema [muzuri] umbo letu, anakumbuka kwamba sisi ni mavumbi.’ (Zaburi 103:14) Kwa hiyo, ikiwa Mungu anajua kama hatuwezi kuepuka kufanya makosa, anatuomba tufanye nini?

Mungu ‘anajua vema [muzuri] umbo letu, anakumbuka kwamba sisi ni mavumbi.’—Zaburi 103:14

NAMNA GANI WANADAMU WASIOKAMILIKA WANAWEZA KUMUFURAHISHA MUNGU?

Shauri lenye Daudi alimupatia mutoto wake Sulemani linatusaidia kuona namna tunaweza kumufurahisha Mungu. Alimushauria hivi: ‘Nawe, Sulemani mwanangu, umujue Mungu wa baba yako, umutumikie kwa moyo kamili.’ (1 Mambo ya Nyakati 28:9) Moyo kamili ni moyo wa namna gani? Ni moyo wenye unamupenda Mungu na unapenda kujua na kufanya mapenzi yake. Haiko moyo mukamilifu, lakini ni moyo wenye unatamani kumutumikia Mungu, kumutii, na wenye kuwa tayari kubadilika. Mungu aliona Ayubu kuwa ‘asiye na lawama,’ Loti kuwa ‘muadilifu,’ na Daudi kuwa mwenye kufanya “yaliyokuwa sawa” machoni pake. Mungu aliwaona hivyo kwa sababu walimupenda na walitamani kumutii. Hata kama walifanya makosa, waliweza kumufurahisha Mungu.

Moyo kamili unapenda kujua mapenzi ya Mungu na unachochewa na tamaa yenye nguvu ya kumutumikia na kumutii

Ikiwa tuko na mawazo mabaya yenye hatungependa yakuwe katika akili yetu, ao tunasikia haya kwa sababu tulisema jambo fulani mbaya, ao ikiwa tulifanya jambo fulani lenye tunaona kama lilikuwa kosa, mifano yenye tumezungumuzia itatusaidia tusivunjike moyo. Mungu anajua kuwa kwa sasa hatuwezi kuwa wakamilifu. Lakini, anatuomba tumupende na tujikaze kumutii. Tukifanya hivyo kwa moyo kamili, tunaweza kuwa hakika kwamba tunaweza pia kumufurahisha Mungu.