Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Maulizo Matatu Yalibadilisha Maisha Yangu

Maulizo Matatu Yalibadilisha Maisha Yangu
  • ALIZALIWA MWAKA WA: 1949

  • INCHI: AMERIKA

  • ALIKUWA: Anatafuta Kujua Kusudi la Maisha

MAISHA YANGU YA ZAMANI:

Nilikomalia Ancram, muji mudogo ulio kaskazini mwa New York, Amerika. Sehemu kubwa ya muji huo ilikuwa mashamba ya kuchungia ngombe wa maziwa. Kwa kweli, ngombe walikuwa wengi kupita watu katika muji huo.

Familia yetu ilikuwa inaenda kwenye kanisa moja tu lenye lilikuwa katika muji. Siku ya Yenga asubuhi, tate (nkambo) mwanaume alikuwa anaangarisha viatu vyangu, kisha nilikuwa ninachukua Biblia nyeupe yenye tate mwanamuke alikuwa amenipatia na kuenda kwenye masomo ya watoto ya Siku ya Yenga. Mimi na wadogo wangu tulifundishwa kutumika kwa bidii, kuheshimia majirani wetu na kuwasaidia, na kuwa wenye shukrani kwa baraka zenye tulipata.

Wakati nilikomaa, niliondoka nyumbani na nikakuwa mwalimu wa masomo. Nilikuwa na maulizo mengi juu ya Mungu na juu ya maisha. Wanafunzi wangu fulani walikuwa na uwezo mwingi. Wengine hawakukuwa na uwezo mwingi lakini walitumika kwa bidii. Wanafunzi fulani walikuwa walemavu, lakini wengine hawakukuwa na ulemavu wowote. Niliona kama hali hiyo haikukuwa ya haki. Wakati fulani wazazi wa wanafunzi wangu wenye hawakukuwa na uwezo mwingi walikuwa wanasema maneno kama haya: “Ni hivi Mungu anapenda mutoto wangu akuwe.” Nilijiuliza sababu gani Mungu aliruhusu watoto fulani wazaliwe na ulemavu. Kwa kweli, mutoto hakufanya kosa lolote.

Pia nilijiuliza, ‘Namna gani ninaweza kutumia muzuri maisha yangu?’ Niliona kama maisha yangu yalikuwa yanapita mbio. Nilikomalia katika familia ya muzuri, nilisomea kwenye masomo za muzuri, na sasa nilikuwa ninafanya kazi yenye nilipenda. Lakini sehemu iliyobaki ya maisha yangu ilionekana kuwa haina kusudi. Mambo tu ningetumaini kufanya, ni kuolewa, kuwa na nyumba ya muzuri na kuzaa watoto, kuendelea kutumika mupaka nifikie miaka ya kuacha kazi, na mwishowe niende katika nyumba ya kuchungia wazee. Nilijiuliza ikiwa maisha iko na kusudi lingine.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU:

Katika kipindi kimoja cha majira ya joto, mimi na walimu fulani wenzangu tulitembelea Ulaya. Tulitembelea kanisa la Westminster, Notre-Dame de Paris, Vatikani, na makanisa mengi madogo-madogo. Niliuliza maulizo yangu kila mahali nilienda. Kisha kurudia nyumbani Sloatsburg, New York, nilitembelea makanisa mengi. Lakini hakuna mutu mwenye alinipatia majibu yenye kusadikisha.

Siku moja, mwanafunzi wangu mumoja aliyekuwa na miaka 12 alinikaribia na kuniuliza maulizo matatu. Kwanza, aliniuliza ikiwa nilijua kuwa yeye ni Shahidi wa Yehova. Nilijibia ndiyo. Pili, aliniuliza ikiwa nilipenda kujua mengi juu ya Mashahidi wa Yehova. Tena, nilijibia ndiyo. Tatu, aliniuliza ninaishi wapi. Wakati nilimupatia adresi yangu, tulitambua kama nilikuwa ninaishi karibu na kwao. Sikujua kama maulizo hayo matatu yenye mutoto mudogo mwanamuke aliniuliza yangebadilisha maisha yangu sikuzote.

Muda mufupi kisha hapo, alikuja na kinga yake nyumbani kwangu na akaanza kunifundisha Biblia. Nilimuuliza maulizo yenye nilikuwa nimeuliza walimu wengi wa dini. Tofauti na walimu hao, yeye alinionyesha majibu yenye kuwa wazi na yenye kusadikisha katika Biblia yangu mwenyewe; nilikuwa sijaona majibu hayo!

Mambo nilijifunza katika Biblia yaliniletea furaha na yalifanya nitosheke. Niliguswa moyo wakati nilisoma andiko la 1 Yohana 5:19, lenye kusema hivi: ‘Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu.’ Nilifurahi kujua kama haiko Mungu ndiye analeta mateso yote yenye tunaona, lakini ni Shetani. Nilifurahi pia kujua kama Mungu atamaliza mateso yote. (Ufunuo 21:3, 4) Nilivumbua kuwa Biblia inaeleweka wakati inafasiriwa waziwazi. Shahidi mwenye alikuwa ananifundisha Biblia alikuwa na miaka 12 tu, lakini niliamini kama kweli ni kweli, hata kama ni nani anaifundisha.

Hata hivyo, nilipenda kuona ikiwa Mashahidi wa Yehova wanaishi kupatana na mambo wanafundisha. Kwa mufano, mutoto huyo mwanamuke alikuwa anakazia kama Wakristo wa kweli wanaonyesha sifa kama vile uvumilivu na fazili. (Wagalatia 5:22, 23) Niliamua kumujaribu ili kuona ikiwa alionyesha sifa hizo. Siku moja nilichelewa kimakusudi kwenye funzo. Nilijiuliza hivi: ‘Ataendelea kuningojea? Na ikiwa ananingojea, atakasirika kwa sababu nimechelewa?’ Wakati nilisimamisha motokari katika njia ndogo ya kuingia kwenye nyumba yangu, nilimuona anangojea mbele ya nyumba. Alikimbia kwenye motokari yangu na kusema hivi: “Nilitaka kurudia nyumbani nimuambie mama yangu tuite kwenye hopitali na polisi ili tujue ikiwa uko muzima, kwa sababu hakuna siku ingine umechelewa kwenye funzo lako. Nilikuwa ninaogopa juu yako!”

Siku ingine, niliuliza ulizo lenye niliwaza kuwa mutoto wa miaka 12 hataweza kujibia. Nilitaka kuona ikiwa atajibia tu kulingana na mawazo yake. Wakati niliuliza ulizo hilo, aliniangalia bila kucheka na kusema hivi: “Hilo ni ulizo ngumu. Nitaliandika kisha nitauliza wazazi wangu.” Na bila shaka, siku iliyofuata alikuja tujifunze, na akaniletea gazeti Munara wa Mulinzi lenye lilikuwa na jibu la ulizo langu. Jambo lenye lilinichochea nipende Mashahidi wa Yehova ni kwamba vichapo vyao vilitoa majibu yenye kutegemea Biblia kwa maulizo yangu yote. Niliendelea kujifunza Biblia na mutoto huyo mwanamuke, na kisha mwaka moja nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. *

FAIDA YENYE NIMEPATA:

Wakati nilipata mwishowe majibu yenye kusadikisha ya maulizo yangu, nilipenda kuyajulisha kila mutu. (Mathayo 12:35) Mwanzoni, watu wa familia yangu walinipinga kwa sababu ya imani yangu mupya. Lakini, kisha wakati fulani upinzani wao ulipunguka. Wakati mama yangu alikaribia kufa, alianza kujifunza Biblia. Hata kama alikufa mbele ya kubatizwa, niko hakika kama alikuwa ameamua kutumikia Yehova.

Katika mwaka wa 1978, niliolewa na Shahidi mumoja anayeitwa Elias Kazan. Katika mwaka wa 1981, mimi na Elias tulialikwa kutumikia kwenye Beteli ya Amerika. * Jambo la kuhuzunisha ni hili: Kisha tu kutumika huko miaka ine, Elias alikufa. Hata kama nilibakia mujane, niliendelea kutumikia kwenye Beteli. Kazi hiyo ilinisaidia nikuwe na jambo la kukazia akili, na ilinifariji kwa kiasi fulani.

Katika mwaka wa 2006, niliolewa tena na Richard Eldred, anayetumikia pia kwenye Beteli.Mimi na Richard tunaendelea kufurahia pendeleo la kutumika kwenye Beteli. Kwa sababu nimejua kweli juu ya Mungu, nimeona kuwa nimepata kabisa majibu ya maulizo yangu, lakini pia maisha yangu yamekuwa na kusudi la kweli. Yote hayo yalianza na maulizo matatu yenye yule mutoto mudogo mwanamuke aliniuliza.

^ fu. 16 Kwa ujumla, mutoto huyo mwanamuke na wakubwa wake, walisaidia walimu 5 kati ya walimu wao wajifunze Biblia na waanze kuabudu Yehova.

^ fu. 18 Neno ‘Beteli’ linamaanisha “Nyumba ya Mungu.” Mashahidi wa Yehova wanatumia neno hilo ili kutaja biro zao za tawi katika inchi mbalimbali. (Mwanzo 28:17, 19) Watu wanaotumikia kwenye Beteli wanafanya kazi mbalimbali zenye zinategemeza kazi ya kufundisha ya Mashahidi wa Yehova.