Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | SERIKALI YENYE HAINA RUSHWA

Ubaya wa Rushwa Katika Serikali

Ubaya wa Rushwa Katika Serikali

Rushwa katika serikali imeelezwa kuwa ni kutumia vibaya mamlaka ya serikali kwa faida ya mutu mwenyewe. Jambo hilo lilianza tangu zamani. Kwa mufano, Biblia ina sheria iliyokataza kupana rushwa katika mambo ya hukumu, hilo linaonyesha kuwa tendo hilo lilikuwa tayari linajulikana muzuri miaka zaidi ya 3500 iliyopita. (Kutoka 23:8) Bila shaka, rushwa inatia ndani mambo mengi zaidi tu ya kukubali kata-midomo (kanyaka, hongo). Wakubwa wa serikali wanaopenda rushwa wakati fulani wanaiba vitu, wanafaidika na kazi fulani zenye hawastahili, ao hata wanaiba feza waziwazi. Wanaweza pia kutumia cheo chao ili kupendelea rafiki wao na watu wa familia zao.

Hata ikiwa rushwa inaweza kupatikana katika kila shirika la watu, inaonekana kuwa rushwa katika serikali ndiyo nyingi sana. Gazeti Global Corruption Barometer la mwaka wa 2013, lililochapishwa na shirika linalochunguza mambo ya rushwa (Transparency International), liliripoti kuwa watu duniani pote wanaona mashirika tano kuwa ndiyo yenye rushwa zaidi. Mashirika hayo ni vyama vya kisiasa, polisi, wakubwa wa serikali, baraza la kutunga sheria, na baraza la kuhukumu watu. Chunguza tu ripoti fulani zinazoonyesha tatizo hilo.

  • AFRIKA: Katika mwaka wa 2013, wakubwa wa serikali 22000 hivi katika Afrika ya Kusini walishitakiwa kuwa na mwenendo mubaya kwa sababu ya matendo ya rushwa.

  • AMERIKA YA KUSINI: Mwaka wa 2012, katika inchi ya Brazili, watu 25 walihukumiwa kwa sababu ya kutumia feza za serikali ili kutafuta kuungwa mukono katika siasa. Kati ya watu waliohukumiwa kulikuwa kiongozi wa zamani wa maofisa wakubwa katika jeshi, aliyekuwa na cheo cha pili katika inchi.

  • ASIA: Katika muji wa Seoul, Korea ya Kusini, watu 502 walikufa wakati duka moja kubwa liliwaangukia katika mwaka wa 1995. Wachunguzi walivumbua kuwa viongozi wa muji huo walikuwa wamepewa rushwa ili kuruhusu wajenzi watumie zege (béton) ya hali mbaya na kuvunja sheria za usalama.

  • ULAYA: Kulingana na Cecilia Malmström, Musimamizi wa Tume ya Ulaya ya Mambo ya Ndani, “Kuenea kwa tatizo hilo [rushwa katika Ulaya] kunashangaza sana.” Aliongezea kuwa “hakuna ahadi kuwa wanasiasa wataondoa rushwa kabisa.”

Rushwa katika serikali ina mizizi mirefu. Profesa Susan Rose-Ackerman, mutu mwenye elimu katika kupiganisha rushwa, aliandika kuwa ili kubadilisha hali inaomba kuwe “mabadiliko makubwa katika namna serikali inafanya kazi.” Hata ikiwa hali hiyo inaweza kuonekana kuwa bila tumaini, Biblia inaonyesha kuwa hata mabadiliko makubwa yanawezekana na kuna uhakika kuwa yatafanywa.