Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Je, inawezekana kuishi milele?

Ni nini kinachoweza kutukomboa kutokana na kifo?

Adamu, mwanaume wa kwanza, aliishi mamia ya miaka. Lakini mwishowe, alizeeka na kufa. Tangu wakati huo, watu wamejaribu njia nyingi ili waepuke kuzeeka. Hata hivyo, hakuna mutu ambaye ameweza kuepuka kifo. Sababu gani? Adamu alizeeka na kufa kwa sababu alifanya zambi kwa kukosa kumutii Mungu. Tunazeeka kwa sababu tumeriti zambi kutoka kwa Adamu na kifo ambacho ni azabu inayotokana na zambi.​—Soma Mwanzo 5:5; Waroma 5:12.

Ili tupate uzima wa milele, tulihitaji mutu fulani alipe zabihu ya ukombozi kwa ajili yetu. (Ayubu 33:24, 25) Zabihu ya ukombozi ni bei inayolipwa ili kumuweka huru mutu aliyekuwa amefungwa, na kwa upande wetu, tulihitaji kufunguliwa kutokana na kifo. (Kutoka 21:29, 30) Yesu alilipa bei hiyo wakati alikufa kwa ajili yetu.​—Soma Yohana 3:16.

Tunaweza kufanya nini ili tupate uzima wa milele?

Si watu wote ambao watakombolewa kutokana na ugonjwa na uzee. Kwa kweli, watu ambao hawamutii Mungu kama Adamu hawatapata pendeleo la kuishi milele. Ni watu tu ambao wanasamehewa zambi zao ndio watapata uzima wa milele.​—Soma Isaya 33:24; 35:3-6.

Ili tusamehewe zambi zetu, tunapaswa kufanya jambo fulani. Ni lazima tumujue Mungu kwa kujifunza Biblia, Neno lake. Biblia inatufundisha namna nzuri ya kuishi na pia namna ya kukubaliwa na Mungu na kupata uzima wa milele.​—Soma Yohana 17:3; Matendo 3:19.