Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UWAFUNDISHE WATOTO WAKO

Tunaweza Kujifunza Nini Kutokana na Mutenda Maovu?

Tunaweza Kujifunza Nini Kutokana na Mutenda Maovu?

Mutenda maovu ambaye tunaweza kujifunza kutokana naye ni yule unayeona kwenye picha akizungumuza na Yesu. Mutenda maovu huyo anasikitika kwa ajili ya matendo yake mabaya. Anamuomba Yesu hivi: “Unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.” Kama unavyoona kwenye picha, Yesu anazungumuza na mutenda maovu huyu. Je, unajua Yesu anamuambia nini? * Yesu anamuahidi hivi: “Kwa kweli mimi nakuambia leo, utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”

Unawaza Paradiso hiyo itakuwa namna gani?— Ili kuhakikisha kwamba tunajibu vizuri, acheni tuzungumuzie Paradiso ambayo Mungu alifanya kwa ajili ya Adamu na Eva, mwanaume na mwanamuke wa kwanza. Paradiso hiyo ilikuwa wapi? Je, ilikuwa mbinguni, ao duniani?

Ikiwa unasema ilikuwa duniani, unajibu vizuri. Kwa hiyo, tunapomuwaza mutenda maovu huyo akiwa “katika Paradiso,” tunapaswa kumufikiria akiishi hapa duniani wakati dunia itakuwa paradiso. Paradiso hiyo itakuwa namna gani?— Acheni tuone.

Kisha Yehova kumuumba Adamu na Eva, mwanaume na mwanamuke wa kwanza, Biblia inasema kwamba aliwatia katika paradiso iliyokuwa tu hapa duniani. Paradiso hiyo iliitwa “bustani ya Edeni.” Unawazia “bustani ya Edeni” ilikuwa namna gani?— Bila shaka, ilikuwa nzuri sana na palikuwa mahali pazuri sana pa kuishi ambapo leo hakuna mutu yeyote amekwisha kuona!

Unawaza namna gani? Je, Yesu atakuwa hapa duniani pamoja na yule mutenda maovu aliyesikitika kwa sababu ya zambi zake?— Hapana, Yesu atakuwa mbinguni akitawala akiwa Mufalme juu ya dunia Paradiso. Kwa hiyo, Yesu atakuwa pamoja na mutenda maovu katika maana ya kwamba atamufufua kutoka kwa wafu na kuhakikisha kuwa anahangaikiwa katika Paradiso duniani. Lakini, sababu gani Yesu ataacha mutu aliyekuwa mutenda maovu aishi katika Paradiso?— Acheni tuzungumuzie jambo hilo.

Ni kweli kwamba mutenda maovu huyo alifanya mambo mabaya sana. Lakini watu wengine wengi walioishi duniani walifanya pia mambo mabaya sana. Hata hivyo, wengi kati yao walifanya mambo mabaya kwa sababu hawakufundishwa hata kidogo juu ya Yehova na juu ya yale alipenda wafanye.

Kwa hiyo watu kama hao, kutia ndani yule mutenda maovu ambaye Yesu alizungumuza naye alipokuwa kwenye muti wa mateso, watafufuliwa na kuishi katika Paradiso hapa duniani. Watafundishwa mapenzi ya Mungu. Na hivyo, wanaweza kuonyesha ikiwa wanamupenda Yehova.

Je, unajua wataonyesha hivyo namna gani?— Kwa kufanya mambo ambayo Mungu anataka wafanye. Litakuwa jambo lenye kupendeza sana kuishi katika Paradiso na kuwa sikuzote pamoja na watu wanaomupenda Yehova na wanaopendana wenyewe!

^ Ikiwa unasoma sehemu hii pamoja na mutoto, unapoona alama hii (—), utue na umutie moyo aeleze mawazo yake.