Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inapatana Kabisa na Mambo ya Kweli ya Sayansi

Biblia Inapatana Kabisa na Mambo ya Kweli ya Sayansi

Biblia Inapatana Kabisa na Mambo ya Kweli ya Sayansi

“Je, kufikia sasa sikukuandikia mashauri na ujuzi, nikuonyeshe ukweli wa maneno ya kweli, ili urudishe maneno yaliyo kweli?”​—METHALI 22:20, 21.

SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Mara nyingi, vitabu vya zamani vina mawazo ya uongo na yenye kuhatarisha maisha ambayo yamekataliwa kabisa na sayansi leo. Hata leo, kwa sababu mambo mapya yanaendelea kuvumbuliwa, waandikaji wanalazimishwa kuandika vitabu vipya ili kurekebisha mawazo yaliyo katika vitabu vyao vya zamani. Lakini Biblia haina lazima ya kurekebishwa kwa sababu ilitoka kwa Muumbaji na Neno lake “linadumu milele.”​—1 Petro 1:25.

KWA MUFANO: Sheria ya Musa iliwaamuru Waisraeli wazike mavi ‘inje ya kambi.’ (Kumbukumbu la Torati 23:12, 13) Ikiwa wangegusa mwili wa munyama aliyekufa ao maiti ya mutu, walipaswa kujisafisha na maji. (Mambo ya Walawi 11:27, 28; Hesabu 19:14-16) Tangu wakati huo, watu wenye ukoma walikuwa wakitengwa na watu wengine mupaka kuhani alipowaangalia na kuhakikisha kama hawawezi tena kuwaambukiza wengine.​—Mambo ya Walawi 13:1-8.

YALE WAGANGA WANASEMA LEO: Leo waganga wanasema kama kuwa na choo ao W.C zinazofaa, kunawa mikono kila mara, na kutenga watu walio na magonjwa ya kuambukiza zingali njia nzuri za kugombanisha magonjwa. Vituo vya Kugombanisha Magonjwa huko Etats-Unis vinatoa mashauri haya: Ikiwa mutu hana W.C ni vizuri afanye choo kubwa kwenye umbali wa metre 30 kutoka mahali palipo na maji na kisha azike mavi yake. Na Shirika la Afya Duniani Pote (OMS) linaonyesha kama ikiwa watu wana choo ao W.C zinazofaa, wanapunguza magonjwa ya kuhara kwa kiasi cha 36%. Kumepita karibu miaka 200, waganga walivumbua kama walikuwa wakiambukiza watu wengi magonjwa kwa sababu hawakuwa wakinawa mikono yao kisha kugusa maiti. Vituo vya États-Unis vya Kugombanisha Magonjwa vinaonyesha kama kunawa mikono kila mara ingali “njia nzuri zaidi inayosaidia watu wasiambukizwe na magonjwa.” Waganga wanasema nini juu ya kutenga watu walio na ukoma ao magonjwa mengine ya kuambukiza? Hivi karibuni, gazeti moja (Saudi Medical Journal) lilisema hivi: “Ugonjwa wa kuambukiza unapoanza, njia moja tu iliyo nzuri zaidi ya kuugombanisha ni kutenga watu walio na ugonjwa huo.”

UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kuna kitabu kingine kitakatifu cha zamani ambacho kina mawazo yenye kupatana na sayansi ya kisasa? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 6]

Kitabu kimoja (MANUAL OF TROPICAL MEDICINE) kilichoandikwa na Muganga ALDO CASTELLANI NA ALBERT CHALMERS kinasema hivi: “Kila mutu anavutiwa kabisa na maagizo juu ya usafi ili kujilinda; maagizo yanayoelezwa katika Sheria ya Musa.”