Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Wajua?

Je, Wajua?

Je, Wajua?

Ni nini “kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili” kinachotajwa mara nyingi katika kitabu cha Kutoka?

Kulingana na simulizi la Biblia, vitambaa vya hema vilivyotumiwa kutengeneza kuta na lango la maskani, yaani, hema la kukutania ambalo lilikuwa kituo cha ibada cha Israeli la kale, vilitengenezwa kwa “uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.” (Kutoka 26:1; 38:18) Nayo “mavazi matakatifu” ya makuhani yalipaswa kutengenezwa kwa “kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili.”—Kutoka 28:1-6.

Kochinili nyekundu, ambayo pia inaitwa kermes, ni rangi nyekundu iliyotengenezwa kutokana na wadudu fulani wa kike wa jamii ya Coccidae. Wadudu hao wasio na mabawa wanaishi kwenye aina fulani ya mti unaoitwa mwaloni (Quercus coccifera), ambao unapatikana Mashariki ya Kati na Pwani ya Mediterania. Rangi hiyo nyekundu inapatikana katika mayai yaliyo ndani ya mwili wa mdudu huyo. Anapokuwa na mayai hayo mwilini mwake, anafanana na tunda jekundu la beri. Mdudu huyo ana ukubwa na umbo kama la njugu, na hukaa kwenye majani au matawi ya mwaloni. Baada ya kuchukuliwa kwa mikono na kupondwa, wadudu hao wanatoa rangi nyekundu, ambayo inaweza kuchanganywa na maji na kutiwa kwenye kitambaa. Mwanahistoria Mroma, Plini Mkubwa, alitaja kochinili nyekundu na aliiona kuwa mojawapo ya rangi zilizothaminiwa zaidi katika siku zake.

Ni waandikaji gani wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ambao walikuwapo siku ya Pentekoste 33 W.K.?

Inawezekana kwamba ni waandikaji sita kati ya waandikaji wanane wa sehemu hiyo ya Maandiko ambao walikuwapo.

Kulingana na simulizi la kitabu cha Matendo, Yesu aliwapa wanafunzi wake agizo hili: “Msiondoke Yerusalemu, bali endeleeni kungojea kile ambacho Baba ameahidi.” (Matendo 1:4) Simulizi hilohilo linaonyesha kwamba Mathayo, Yohana, na Petro ambao baadaye wangekuwa waandikaji wa Biblia, walitii agizo hilo na kukusanyika “mahali palepale” pamoja na wanafunzi wengine. Ndugu wa kambo wa Yesu walikuwapo pia. (Matendo 1:12-14; 2:1-4) Baadaye, wawili kati yao, Yakobo na Yuda (Yudasi), waliandika vitabu viwili vya Biblia ambavyo vinaitwa kwa majina yao.—Mathayo 13:55; Yakobo 1:1; Yuda 1.

Katika kitabu chake cha Injili, Marko anataja mwanamume kijana aliyekimbia ule usiku ambao Yesu alikamatwa. Inaelekea alikuwa akijirejelea, kwa kuwa wanafunzi wengine wote walikuwa wamemwacha Yesu. (Marko 14:50-52) Kwa hiyo, yaelekea Marko alikuwa mwanafunzi wa mapema, na inawezekana alikuwapo siku ya Pentekoste.

Waandikaji wawili wanaobaki wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ambayo yameongozwa na roho ya Mungu ni Paulo na Luka. Siku ya Pentekoste 33 W.K., Paulo hakuwa mfuasi wa Kristo. (Wagalatia 1:17, 18) Yaonekana Luka hakuwapo pia, kwa kuwa hajitaji kati ya “mashahidi” waliojionea huduma ya Yesu.—Luka 1:1-3.

[Picha katika ukurasa wa 22]

Wadudu waliotumiwa kutayarisha rangi

[Hisani ya Picha]

Courtesy of SDC Colour Experience (www.sdc.org.uk)

[Picha katika ukurasa wa 22]

Petro akizungumza siku ya Pentekoste 33 W.K.