Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uamuzi Niliochukua Nilipokuwa Kijana Mudogo

Uamuzi Niliochukua Nilipokuwa Kijana Mudogo

Nilipokuwa kijana mudogo

Nilikuwa na miaka kumi tu katika 1985 wakati watoto fulani kutoka Kambuchea (Cambodge) walihamia kwenye masomo yangu huko Columbus, Ohio, Amerika. Kijana mumoja kati yao alijua maneno machache ya Kiingereza. Kwa kutumia picha, alianza kunielezea hadisi zenye kuogopesha za watu waliokuwa wakitesa wengine, wakiwaua, na kutoroka. Nililalamika usiku nilipokumbuka watoto hao. Nilitamani kuwaelezea juu ya ahadi ya Paradiso na ufufuo, lakini hawakuelewa luga yangu. Ijapokuwa nilikuwa kijana mudogo tu, niliamua kujifunza luga ya Kambuchea ili niweze kuelezea wanafunzi wenzangu kuhusu Yehova. Wakati huo sikujua kabisa kwamba uamuzi huo ungebadili maisha yangu.

Haikuwa rahisi kujifunza luga ya Kambuchea. Niliamua mara mbili kuacha kujifunza, lakini Yehova alinitia moyo kupitia wazazi wangu. Baadaye, walimu wangu na wanafunzi wenzangu walianza kunitia moyo nitafute kazi nzuri. Lakini nilitaka kuwa painia, kwa hiyo nilichagua masomo ambayo yangeniwezesha kupata kazi isiyochukua wakati mwingi ili niweze kufikia muradi wangu. Kisha masomo, nilizoea kuenda kukutana na mapainia fulani na kuhubiri pamoja nao. Niliamua kuwafundisha nyumbani wanafunzi waliokuwa wakijifunza Kiingereza​—uamuzi huo uliniletea faida nyingi baadaye.

Nilipokuwa na miaka 16, nilisikia kwamba kuna kikundi cha luga ya Kambuchea huko Long Beach, California, Amerika. Nilitembelea huko na nilijifunza kusoma luga ya Kambuchea. Kisha tu kumaliza masomo, nilikuwa painia na niliendelea kuwahubiri watu wanaozungumuza luga ya Kambuchea walioishi karibu na kwetu. Nilipokuwa na miaka 18, nilikuwa nikifikiria kuhamia Kambuchea. Ilikuwa mahali hatari, lakini nilijua kwamba wengi kati ya watu milioni kumi wanaoishi huko Kambuchea walikuwa hawajasikia habari njema ya Ufalme. Wakati huo, kulikuwa kutaniko moja tu lenye wahubiri 13 katika Kambuchea yote. Nilipokuwa na miaka 19, nilitembelea Kambuchea kwa mara ya kwanza. Kisha miaka miwili, niliamua kuenda kuishi huko. Nilipata kazi ya muda ya kutafsiri na kufundisha Kiingereza ili kutosheleza mahitaji yangu. Baadaye, nilipata bibi aliyekuwa na miradi kama yangu. Tumefurahia pamoja kusaidia watu wengi wa Kambuchea wajitoe kwa Mungu.

Yehova amejibu ‘maombi ya moyo wangu.’ (Zab. 37:4) Hakuna kazi inayoleta furaha kubwa kama vile kazi ya kuhubiri. Kwa miaka 16 ambayo nimepitisha huko Kambuchea, kikundi hicho kidogo cha wahubiri 13 kimezaa makutaniko 12 na vikundi 4 vya maeneo ya mashambani!​—Imesimuliwa na Jason Blackwell.