Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Usikate Tumaini Hata Kidogo!

Usikate Tumaini Hata Kidogo!

Je, wewe ni Shahidi wa Yehova wa miaka mingi na ungependa mwenzi wako wa ndoa amuabudu Yehova pamoja nawe?

Ao je, umevunjika moyo kwa sababu mutu uliyejifunza naye Biblia, ambaye alionyesha kupendezwa sana amerudi nyuma?

Mambo fulani ambayo wahubiri kutoka Grande-Bretagne walikutana nayo yatakuonyesha kwa nini haupaswe kukata tumaini hata kidogo. Utaona pia yale unayoweza kufanya ili ‘kutupa mukate wako juu ya uso wa maji,’ ni kusema, kusaidia wale ambao hawajakubali kweli.—Mhu. 11:1.

UVUMILIVU NI WA MAANA SANA

Sifa ya maana sana unayopaswa kuwa nayo ni uvumilivu. Unapaswa kushikamana sana na kweli na Yehova pia. (Kum. 10:20) Hilo ndilo jambo ambalo dada Georgina alifanya. Alianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova katika mwaka wa 1970, bwana yake, Kyriacos, alikasirika sana. Alijaribu kumukataza kujifunza, hakukubali Mashahidi wa Yehova waingie katika nyumba yake, na alikuwa anatupa vitabu vya Mashahidi wa Yehova ambavyo alikuwa anapata.

Dada Georgina alipoanza kuhuzuria mikutano, Kyriacos akasirika hata zaidi. Siku moja alienda kwenye Jumba la Ufalme ili kuanzisha ubishi. Dada mumoja alipotambua kama Kyriacos anazungumuza Kigiriki vizuri kuliko Kiingereza, alimuita ndugu mumoja Mugiriki wa kutaniko lingine kwa njia ya telefone ili aje kuwasaidia. Kyriacos alizungumuza kwa adabu na ndugu huyo, na kisha miezi michache, walianza hata kujifunza Biblia pamoja. Lakini, kisha Kyriacos aliacha kujifunza.

Dada Georgina akaendelea kupambana na mateso kwa miaka mingine mitatu. Kyriacos alimuambia kwamba ikiwa anabatizwa, ataachana naye. Siku ya ubatizo wake, Georgina alisali sana kwa Yehova ili Kyriacos asimuache. Wakati Mashahidi wa Yehova walikuja kumuchukua ili waende kwenye mukusanyiko, Kyriacos aliwaambia hivi: “Mutangulie. Tutawafuata katika motokari yetu.” Alihuzuria kipindi cha asubuhi cha mukusanyiko na ubatizo wa bibi yake!

Karibu miaka 40 kisha dada Georgina kukutana na Mashahidi wa Yehova, bwana yake alibatizwa

Kisha hapo, upinzani wa Kyriacos ukapunguka, na akaanza kufanya mabadiliko makubwa. Karibu miaka 40 kisha Georgina kukutana na Mashahidi wa Yehova, bwana yake alibatizwa. Ni jambo gani lililomusaidia Kyriacos? Yeye anasema hivi: “Nilifurahia sana Georgina kwa sababu alishikamana na Yehova.” Georgina anasema hivi: “Ijapokuwa bwana yangu alikuwa ananitesa, sikuacha kumuabudu Mungu wangu hata kidogo. Muda wote huo niliendelea kusali kwa Yehova, na sikukata tumaini hata kidogo.”

UTU MUPYA NI WA MAANA SANA

Jambo lingine linaloweza kusaidia bibi ao bwana yako ni sifa za Kikristo unazoonyesha. Mutume Petro alishauri wanawake Wakristo hivi: “Jitiisheni kwa waume zenu wenyewe, ili, ikiwa wowote si watiifu kwa lile neno, wavutwe bila neno kupitia mwenendo wa wake zao.” (1 Pet. 3:1) Dada Christine alitumia shauri hilo, hata ikiwa ilichukua miaka mingi ili amuvute bwana yake. Alipokuwa Shahidi wa Yehova miaka zaidi ya 20, bwana yake John hakuona ulazima wa Mungu katika maisha yake. John hakupenda mambo ya dini, lakini alitambua kwamba Christine alipendezwa sana na dini yake mupya. Anasema hivi: “Niliona kwamba dini hiyo ilimufanya awe mwenye furaha na mwenye sifa nyingi nzuri, na hilo lilinisaidia nipambane na matatizo mengi.”

Dada Christine hakumukaza hata kidogo bwana yake akubali dini yake, bwana yake anasema hivi: “Christine alitambua kwamba haikuwa vizuri azungumuze nami kuhusu dini yake, na kwa uvumilivu aliniacha nijifunze polepole na kwa namna yangu.” Christine alipoona katika magazeti Munara wa Mulinzi ao Amkeni! habari fulani ambayo alijua kama inaweza kumupendeza John, kama vile habari za siyanse na uumbaji, alimuonyesha habari hiyo na kumuambia: “Nawaza utapenda kusoma habari hii.”

Kisha, John alipata pansyo na akaanza kufanya kazi ya kutengeneza bustani. Kwa kuwa alikuwa na wakati mwingi wa kufikiri juu ya maulizo yanayohusu uzima, alianza kufikiri hivi: “Je, wanadamu wako duniani kwa bahati tu, ao tuliumbwa kwa kusudi fulani?” Siku moja, ndugu mumoja aliyekuwa akizungumuza na John kupitia Internete alimuuliza John hivi: “Unawaza nini kuhusu kujifunza Biblia?” John akamuambia: “Sasa kwa kuwa nimeanza kumuamini Mungu, ninakubali tuanze kujifunza Biblia nawe.”

Dada Christine alifanya vizuri sana kwa sababu hakukata tumaini! Kisha kusali kwa muda wa miaka 20 ili Mungu amusaidie John akubali kweli, John alibatizwa. Sasa wanamutumikia Yehova pamoja kwa bidii. John anatambua hili: “Kuna mambo mawili yaliyonivuta, ni kusema, wema na urafiki wa Mashahidi wa Yehova. Na unapokuwa na bibi ao bwana Shahidi wa Yehova, una mwenzi mwaminifu, mwenye kutumainiwa na mwenye kujinyima.” Kwa kweli, Dada Christine alitumikisha maneno yaliyo kwenye 1 Petro 3:1, na yakawa na matokeo mazuri!

MBEGU ZITAOTA HATA KISHA MIAKA MINGI

Namna gani ikiwa watu fulani waliojifunza Biblia hawapendezwe tena kwa sababu fulani? ‘Asubuhi panda mbegu zako na mupaka jioni usiache mukono wako upumuzike; kwa maana haujue ni wapi hii itafanikiwa, hapa ao pale, ao ikiwa zote mbili zitakuwa njema.’ (Mhu. 11:6) Mara nyingine inachukua miaka mingi ili mbegu ya kweli iliyopandwa katika moyo wa mutu ianze kuota. Hata hivyo, mwishowe mutu anaweza kufikia kuona umaana wa kumukaribia Mungu. (Yak. 4:8) Ndiyo, siku fulani mutu huyo anaweza kufanya uamuzi ambao utakushangaza na kukufurahisha.

Fikiria dada Alice, aliyetoka India na kuhamia Angleterre. Alianza kujifunza Biblia katika 1974. Alizungumuza Kihindi, lakini alipenda kujua Kiingereza vizuri. Aliendelea kujifunza kwa muda wa miaka fulani, kisha akaanza kuhuzuria mikutano fulani katika kutaniko moja linalotumia luga ya Kiingereza. Alijua kama alikuwa anajifunza mambo ya kweli, lakini hakuyachukua kwa uzito. Tena alipenda feza sana na alipenda mambo ya karamu sana. Mwishowe, akaacha kujifunza.

Kisha miaka karibu 30, dada Stella, aliyekuwa anajifunza na Alice, alipokea barua kutoka kwake. Inasomwa hivi: “Niko hakika kwamba utafurahi kusikia kama mutu uliyekuwa unajifunza naye Biblia kuanzia mwaka wa 1974 amebatizwa kwenye mukusanyiko wa wilaya uliofanywa hivi karibuni. Ulifanya kazi ya maana sana katika maisha yangu. Ulipanda mbegu katika moyo wangu, hata ikiwa wakati huo sikuwa tayari kujitoa kwa Mungu, lakini niliendelea kuweka mbegu hiyo ya kweli katika akili na moyo wangu.”

Barua ambayo Alice alimutumia Stella inasomwa hivi: “Niko hakika kwamba utafurahi kusikia kama mutu uliyekuwa unajifunza naye Biblia kuanzia mwaka wa 1974 amebatizwa kwenye mukusanyiko wa wilaya uliofanywa hivi karibuni”

Ni jambo gani lilitokea? Alice anaeleza kwamba alikuwa mwenye huzuni sana wakati bwana yake alipokufa katika mwaka wa 1997. Dakika kumi kisha kusali kwa Mungu, Mashahidi wa Yehova wawili wanaozungumuza luga ya Punjabi walimutembelea na kumuachia trakte Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa? Alice akaona kwamba sala yake ilijibiwa na akaamua kutafuta Mashahidi wa Yehova. Lakini, angewapata wapi? Alipata adresi ya kutaniko la luga ya Punjabi ambayo Stella alimupatia hapo zamani. Alice akaenda kwenye Jumba la Ufalme na akakaribishwa kwa uchangamufu na ndugu na dada waliozungumuza luga hiyo. Alice anasema hivi: “Nilijisikia kama waliendelea kunipenda na hilo lilinisaidia nishinde huzuni yangu.”

Alianza kukusanyika kwa ukawaida na akarudilia tena kujifunza Biblia, akajifunza kuzungumuza luga ya Punjabi na kuisoma vizuri sana. Katika mwaka wa 2003 alibatizwa. Katika barua aliyomutumia Stella anamalizia hivi: “Asante sana kwa kupanda mbegu hiyo kumepita miaka 29 na kuniachia mufano muzuri wa kufuata.”

“Asante sana kwa kupanda mbegu hiyo kumepita miaka 29 na kuniachia mufano muzuri wa kufuata.”​—Alice

Unaweza kujifunza nini kutokana na habari hizo? Muda murefu unaweza kupita, lakini ikiwa mutu ana njaa ya kiroho, ikiwa mutu ni mwenye moyo wa haki, na ikiwa ni munyenyekevu, Yehova ataruhusu kweli iliyopandwa katika moyo wake ikomae. Kumbuka maneno haya katika mufano wa Yesu: ‘Ile mbegu huota na hukua na kuwa ndefu, naye [mupandaji] hajue ni jinsi gani hasa. Udongo wenyewe hutokeza matunda hatua kwa hatua, kwanza jani, kisha suke, mwishowe nafaka iliyo kamili katika suke.’ (Mk. 4:27, 28) Ukuzi huo unafanyika polepole na kutokea ‘wenyewe.’ Kwa kweli, kila muhubiri wa Ufalme hajue namna gani hilo linatokea. Kwa hiyo, endelea kupanda mbegu kwa uwingi. Unaweza kuvuna kwa uwingi.

Na usisahau umaana wa sala. Dada Georgina na Christine waliendelea kusali kwa Yehova. Ikiwa ‘unadumu katika sala’ na haukate tumaini, “baada ya siku nyingi,” unaweza kupata tena ‘mukate’ ambao ulitupa juu ya uso wa maji.​—Rom. 12:12; Mhu. 11:1.