Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | BIBLIA ILIOKOKA NAMNA GANI?

Biblia Iliokoka Hatari ya Kuharibika

Biblia Iliokoka Hatari ya Kuharibika

HATARI: Zamani, waandikaji wa Biblia na wale wenye walifanya kopi ya maandishi ya Biblia walitumia mafunjo * na ngozi za nyama. (2 Timotheo 4:13) Namna gani mafunjo na ngozi za nyama vilitia Biblia katika hatari?

Mafunjo yanapasuka, yanapoteza rangi, na yanaregea haraka. Richard Parkinson na Stephen Quirke, wanasayansi wenye kujifunza mambo ya zamani ya Misri, wanasema hivi: “Kisha muda fulani, karatasi ya mafunjo inaweza kuanza kuharibika na kuwa kamba-kamba na kufikia kuwa vumbi. Wakati kitabu cha kukunjwa kinawekwa, kinaweza kuanza kuharibika ao kuoza kwa sababu ya baridi na kinaweza kukuliwa na panya ao vidudu, zaidi sana siafu wa rangi ya mweupe kama kinapatikana katika udongo.” Kisha kuvumbuliwa, mafunjo fulani yaliwekwa kwenye mwangaza mukubwa wa jua ao baridi kali, na hilo lilifanya mafunjo hayo yaharibike haraka.

Ngozi za nyama zinakawia kuliko mafunjo, lakini zinaharibika pia kama zinatumiwa mubaya ao kama zinawekwa nafasi ya kifukutu ao ya baridi sana, na nafasi ya mwangaza mukubwa wa jua. * Ngozi ya nyama inaweza pia kukuliwa na vidudu. Ndiyo sababu kitabu kimoja kinasema hivi: “Ni nguvu sana maandishi ya zamani kuokoka.” (Everyday Writing in the Graeco-Roman East) Kama mafunjo ao ngozi za nyama zenye kuwa na maandishi ya Biblia zingeharibika, ujumbe wa Biblia ungepotea pia.

NAMNA BIBLIA ILIOKOKA: Sheria ya Wayahudi ililazimisha kila mufalme ‘ajiandikie katika kitabu nakala ya Sheria hii,’ ni kusema, vitabu tano vya kwanza vya Biblia. (Kumbukumbu la Torati 17:18) Zaidi ya hilo, watu wenye kujua kufanya kopi waliandika kopi nyingi sana za maandishi kati ya mwaka wa 1 na 100 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Kwa hiyo, Maandiko yangeweza kupatikana katika masinagogi ya Israeli yote na hata mbali katika Makedonia! (Luka 4:16, 17; Matendo 17:11) Sababu gani maandishi fulani ya zamani sana yanapatikana mupaka leo?

Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi vimefanya mamia ya miaka bila kuharibika ndani ya mitungi ao ndani ya shimo nafasi yenye kukauka

Philip Comfort, mwenye elimu ya Agano Jipya anasema hivi: “Wayahudi walijulikana kuwa watu wenye kuweka vitabu vya kukunjwa katika mitungi ili kuvilinda. Inawezekana Wakristo waliendelea pia na tabia hiyo. Ndiyo sababu maandishi fulani ya zamani ya Biblia yalivumbuliwa katika vyombo vya udongo, katika vyumba vidogo-vidogo, ndani ya mashimo, na mara fulani tu kwenye kukauka.

MATOKEO: Maelfu ya sehemu ya maandishi ya Biblia yanapatikana mupaka leo. Maandishi fulani kati ya maandishi hayo yamefanya zaidi ya miaka 2000. Hakuna kitabu cha zamani chenye kuwa na maandishi mengi ya zamani sana kama Biblia.

^ fu. 3 Mafunjo (papyrus) ni karatasi zenye zilitengezwa kupitia mumea wenye kuitwa funjo. Mumea huo unaota nafasi kwenye kuwa maji.

^ fu. 5 Kwa mufano, Tangazo la Uhuru wa inchi ya États-Unis liliandikwa kwenye ngozi ya nyama. Sasa, kumepita karibu miaka 250 kisha tangazo hilo kuandikwa; lakini ngozi hiyo imepoteza rangi yake na kufanya ikuwe nguvu kusoma maandishi yenye kuwa ndani.