Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaweza Kusali Namna Gani Juu Mungu Akusikie?

Unaweza Kusali Namna Gani Juu Mungu Akusikie?

Yehova Mungu ni “Musikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2) Tunaweza kuzungumuza naye fasi yoyote na wakati wowote, kwa sauti ao bila sauti. Wakati tuko tunasali, Yehova anapenda tumuite “Baba,” na ni Baba wa muzuri zaidi mwenye tunaweza kuwa naye. (Matayo 6:9) Kwa upendo Yehova anatufundisha namna tunaweza kusali kwake ili atusikie.

SALI KWA YEHOVA MUNGU KATIKA JINA LA YESU

“Kama munamuomba Baba jambo lolote, atawapatia ninyi katika jina langu.”​Yohana 16:23.

Maneno ya Yesu inaonyesha waziwazi kama Yehova anapenda tusali kwake katika jina la Yesu Kristo, hapana kupitia sanamu, watakatifu, malaika, ao wazazi wa zamani wenye wamekufa. Wakati tunasali kwa Mungu katika jina la Yesu, tunaonyesha kama tunaelewa daraka la maana lenye Yesu iko nalo. Yesu alisema hivi: “Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.”​—Yohana 14:6.

ZUNGUMUZA KUTOKA KATIKA MOYO

“Mumwange mioyo yenu mbele yake.”​—Zaburi 62:8.

Wakati tunasali kwa Yehova, tunapaswa kuzungumuza naye kama vile mutoto anazungumuzaka na baba yake mwenye upendo. Kuliko kusoma sala mu kitabu ao kurudilia sala yenye tulishachunga mu akili, tunapaswa kuzungumuza naye kwa heshima na kutoka katika moyo.

SALI KULINGANA NA MAPENZI YA MUNGU

“Hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.”​—1 Yohana 5:14.

Mu Biblia, Yehova Mungu anatuambia mambo yenye atatufanyia na anatuambia mambo yenye anapenda tumufanyie. Ili Mungu akubali sala zetu, tunapaswa kusali “kulingana na mapenzi yake.” Juu tufikie kufanya vile, tunapaswa kujifunza Biblia ili tumujue muzuri. Kama tunamujua muzuri, sala zetu zitamufurahisha.

TUNAWEZA KUSALI JUU YA MAMBO GANI?

Usali Juu ya Mambo Yenye Uko Nayo Lazima. Tunaweza kusali kwa Mungu juu ya mahitaji yetu ya kila siku, kama vile chakula, nguo, na fasi ya kuishi. Tunaweza pia kumuomba Mungu atupatie hekima ya kukamata maamuzi ya muzuri na kumuomba atupatie nguvu ili tuvumilie magumu. Tunaweza kumuomba Mungu atupatie imani, atusaidie, na atusamehe makosa yetu.​—Luka 11:3, 4, 13; Yakobo 1:5, 17.

Usali kwa Ajili ya Wengine. Wazazi wenye wanapenda watoto wao wanajisikiaka muzuri wakati watoto wao wanapendana. Yehova pia anafurahi wakati watoto wake ku dunia wanahangaikiana. Ni muzuri kusali kwa ajili ya bwana ao bibi yetu, watoto wetu, familia yetu, na marafiki wetu. Mwanafunzi Yakobo anatutia moyo “kusali kwa ajili ya mutu na mwenzake.”​—Yakobo 5:16.

Uonyeshe Shukrani. Juu ya Muumbaji wetu, Biblia inasema hivi: “Kwa kutenda mema, aliwapatia ninyi mvua kutoka mbinguni na vipindi vya kuzaa matunda, na kuwapatia chakula kwa wingi na kujaza mioyo yenu furaha.” (Matendo 14:17) Wakati tunafikiria mambo yote yenye Mungu ametufanyia, ile inatuchochea tumushukuru katika sala. Bila shaka, tunapaswa pia kuonyesha shukrani yetu kwa Mungu kupitia namna yetu ya kuishi.​—Wakolosai 3:15.

UKUWE MUVUMILIVU NA UENDELEE KUSALI

Wakati fulani, tunaweza kujisikia mubaya wakati sala zetu zenye kutoka katika moyo hazipate jibu mara moja. Ile inamaanisha kama Mungu hatuhangaikiake? Hapana! Fikiria mufano wenye kufuata wenye unaonyesha kama ni muzuri kuendelea kusali.

Steve, mwenye tulizungumuzia katika habari ya kwanza, anasema hivi: “Ikiwa sikuendelea kusali, ningepoteza tumaini langu lote la kuwa tena na furaha.” Nini njo ilimusaidia? Wakati alianza kujifunza Biblia, alielewa kama ni jambo la maana kusali na kuendelea kusali. Steve anasema hivi: “Ninatoaka sala kwa Mungu ili kumushukuru kwa musaada wote wenye upendo wenye nilipata kupitia marafiki wangu wapendwa. Leo niko mwenye furaha zaidi.”

Tuseme nini juu ya Jenny, mwenye alijiona kuwa wa bure na kuwaza kama Mungu hawezi kusikia sala zake? Anasema hivi: “Wakati nilijisikia kuwa mutu wa bure sana, nilisali kwa Mungu ili anisaidie nielewe juu ya nini nilikuwa ninajisikia vile.” Kufanya vile kulimuletea faida gani? “Kuzungumuza na Mungu katika sala kumenisaidia nijione kama vile ananiona, ni kusema, nielewe kuwa hata kama moyo wangu unanihukumu, Mungu hanihukumu. Kumenisaidia pia niendelee kusali.” Alipata matokeo gani? “Sala imenisaidia nione Yehova kuwa mutu wa kweli, mwenye upendo, mwenye kuhangaikia watu, Baba, na Rafiki; mwenye sikuzote ananisaidia wakati ninaendelea kufanya mapenzi yake.”

Wakati Isabel anaona namna mutoto wake Gerard anafurahia maisha hata kama ni kilema anasema, “Ninaelewa kama mutoto wangu njo jibu la muzuri zaidi la sala zangu”

Fikiria pia mufano wa Isabel. Wakati alikuwa na mimba, munganga wake alimuambia kama atazaa mutoto mwenye kuwa na ulemavu wa nguvu. Alihuzunika sana. Watu fulani walimushauria hata atoshe ile mimba. “Niliwaza kama ile huzuni itaniua.” Alifanya nini? Alisema hivi: “Nilisali sana kwa Mungu ili kumuomba musaada.” Alifikia kuzaa mutoto mwanaume, Gerard, na alikuwa kilema. Isabel anajisikia kama Mungu alijibia sala zake? Ndiyo! Namna gani? Isabel anasema hivi: “Wakati ninaona mutoto wangu, mwenye iko sasa na miaka 14, anafurahia maisha hata kama ni kilema, ninaelewa kama mutoto wangu njo jibu la muzuri zaidi la sala zangu na ni baraka kubwa zaidi kutoka kwa Yehova Mungu.”

Maneno ya vile yenye kutoka katika moyo, inatufanya tufikirie maneno ya muandikaji mumoja wa zaburi mwenye alisema hivi: “Utasikia ombi la wapole, Ee Yehova. Utafanya mioyo yao kuwa imara na utawakazia sana uangalifu.” (Zaburi 10:17) Zile ni sababu za muzuri sana zenye zinatusaidia tuendelee kusali kwa Mungu!

Mu Biblia munapatikana sala mingi zenye Yesu alitoa. Bila shaka sala yenye kujulikana sana ni ile yenye alifundisha wanafunzi wake. Tunaweza kujifunza nini kupitia ile sala?