Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUFANYA AMANI KATIKA NYUMBA YENU

Kukosana Katika Nyumba—Kunatokea Namna Gani?

Kukosana Katika Nyumba—Kunatokea Namna Gani?

SARAH* wa inchi ya Ghana, mwenye ameolewa na Jacob kwa miaka 17, anasema hivi: “Mara nyingi tunakosana juu ya feza.” Anaeleza hivi: “Ninajisikia kuwa mwenye kasirani kwa sababu ninafanya yangu yote ili kutunza familia lakini Jacob hazungumuze na mimi hata siku moja juu ya feza zetu. Tunafanyaka majuma bila kuzungumuza.”

Jacob, bwana yake, anasema hivi: “Ndiyo, kuko wakati tunatupiana maneno makali. Mara nyingi inakuwa hivyo kwa sababu ya kukosa kuelewana na kukosa mazungumuzo ya muzuri. Kukosana kunatokea pia kwa sababu ya kukasirika kupita kiasi katika hali mbalimbali.”

Nathan, wa inchi ya India, mwenye hajakawia katika ndoa, anaeleza jambo lenye lilitokea siku moja wakati baba-mukwe wake alimufokea mama-mukwe wake. Anasema hivi: “Mama-mukwe alikasirika na kuondoka nyumbani. Wakati nilimuuliza baba-mukwe wangu sababu gani alimufokea vile, aliona kama mimi mutoto wake mukwe nilikuwa ninamutukana yeye. Kisha hapo, alianza kutufokea sisi wote.”

Pengine wewe pia umeona namna maneno mabaya ao yenye kutumiwa kwa wakati wenye haustahili, yanaweza kufanya watu wakosane sana katika nyumba. Mazungumuzo yenye kuanza kwa upole yanaweza kugeuka haraka na kuwa vita ya maneno. Hakuna mutu mwenye anaweza kusema mambo yenye kuwa sawa wakati wote, kwa hiyo, inaweza kuwa vyepesi kuelewa mubaya maneno ya wengine ao nia zao. Lakini, inawezekana kuwa na amani na upatano.

Unaweza kufanya nini wakati mabishano makali yanatokea? Unaweza kufanya nini ili kurudisha amani na utulivu katika nyumba? Namna gani familia zinaweza kuendeleza amani katika nyumba zao? Tafazali, endelea kusoma habari zenye kufuata.

Majina fulani yamebadilishwa katika habari hizi.