Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo Unapaswa Kujua Juu ya Malaria

Mambo Unapaswa Kujua Juu ya Malaria

Shirika la Afya Ulimwenguni (OMS) linakadiria kuwa, katika mwaka wa 2013, watu zaidi ya milioni 198 walipata ugonjwa wa malaria, na watu karibu 584000 walikufa kwa sababu ya ugonjwa huo. Kati ya kila watu 5 wenye walikufa kwa sababu ya Malaria, watu karibu 4 walikuwa watoto wa chini ya miaka tano. Ugonjwa huo unatesa watu katika inchi na maeneo karibu 100 duniani pote, na kwa hiyo unahatarisha maisha ya watu miliare 3 na milioni 200 hivi.

1 MALARIA NI NINI?

Malaria ni ugonjwa wenye kuletwa na mikrobe yenye inaingizwa katika mwili. Kati ya alama zenye kuonyesha kuwa mutu iko na malaria kuna homa (fièvre), baridi, kutokwa jasho, maumivu ya kichwa, maumivu ya mwili, kichefuchefu (nausée), na kutapika. Wakati fulani, alama za malaria zinaweza kurudia kisha kila saa 48 mupaka 72, kulingana na aina ya mikrobe ya malaria yenye mutu iko nayo ao kulingana na wakati wenye mutu amefanya na ugonjwa huo.

2 NAMNA GANI MUTU ANAPATA MALARIA?

  1. Mikrobe ya malaria yenye kuitwa Plasmodia inaingizwa katika damu ya mutu wakati anaumwa na imbu wa kike wa aina ya Anophèles.

  2. Mikrobe hiyo inaingia katika chembe za maini ya mutu, na humo inaanza kuongezeka.

  3. Wakati chembe ya maini inapasuka, mikrobe hiyo inatoka, kisha inashambulia chembe nyekundu za damu. Kisha mikrobe hiyo inaendelea kuongezeka katika chembe nyekundu.

  4. Wakati chembe nyekundu ya damu inapasuka, inatoa mikrobe hiyo, na inashambulia chembe zingine nyekundu.

  5. Chembe nyekundu za damu zinaendelea kushambuliwa na kupasuka. Kwa kawaida mutu anaonyesha alama za malaria kila wakati chembe nyekundu za damu zinapasuka.

3 NAMNA UNAWEZA KUJILINDA

Ikiwa unaishi katika inchi yenye kuwa sana na malaria . . .

  • Utumie mustikere. Mustikere hiyo inapaswa kuwa:

    • yenye kutiwa dawa ya kuua vidudu.

    • bila tundu ao nafasi yenye kupasuka.

    • yenye kuingizwa muzuri chini ya matelas.

  • Tumikisha dawa ya kupulizia katika nyumba ili kuua vidudu.

  • Ikiwezekana, uweke mustikere kwenye milango na madirisha, na utumie mashine za kutia hewa katika nyumba, kwa sababu zinafukuza imbu.

  • Uvae nguo zenye rangi yenye kungaa zenye kufunika muzuri mwili wako.

  • Ikiwa inawezekana, uepuke kuwa nafasi yenye miti ao majani mengi, kwa sababu imbu wengi wanaishi hapo, ao nafasi yenye kuwa na maji yasiyoteremuka kwa sababu wanataga mayai hapo.

  • Ikiwa unapata malaria, utafute matunzo bila kukawia.

Ikiwa unapanga kusafiri katika inchi yenye kuwa sana na malaria . . .

  • Utafute habari za hivi karibuni mbele ya kusafiri. Aina ya mikrobe ya malaria katika inchi moja inaweza kuwa tofauti na mikrobe yenye kuwa katika inchi ingine, na hilo linasaidia kujua ni dawa gani inaweza kuwa ya muzuri zaidi. Tena, umuulize muganga ni mambo gani unapaswa kujua, kwa kufikiria magonjwa yenye yamekwisha kukupata.

  • Wakati uko katika inchi hiyo, utumikishe mambo yenye kutajwa katika habari hii kwa ajili ya watu wenye kuishi katika inchi zenye kuwa sana na malaria.

  • Ikiwa unapata malaria, utafute matunzo bila kukawia. Ujue kama alama za malaria zinaweza kuonekana juma moja ao juma mbili kisha kupata ugonjwa huo.