Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA

Mungu Anakuwaka? Faida 4 za Kujua Hivyo

Mungu Anakuwaka? Faida 4 za Kujua Hivyo

Watu wengi wanaona kuwa ulizo la kujua ikiwa Mungu anakuwaka halina jibu ao halina maana. Hervé, mwenye alikomalia katika inchi ya Ufaransa, anasema hivi: “Mimi siamini kama Mungu hakuwake ao kama mambo ya Mungu hayajulikane, lakini sina dini. Mimi ninaona kuwa njia ya muzuri ya kuishi ni kutumikisha akili. Na sina lazima ya musaada wa Mungu ili kufanya maamuzi mazuri.”

Watu wengine wanaweza kuwa kama John, wa inchi ya Amerika. Alisema hivi: “Nililelewa na wazazi wenye hawakuamini Mungu. Wakati nilikuwa kijana, sikukuwa ninajua ikiwa Mungu anakuwaka ao hapana. Lakini, wakati fulani nilikuwa ninawaza juu ya jambo hilo.”

Umekwisha kujiuliza ikiwa Mungu anakuwaka, na ikiwa anakuwaka, maisha yana kusudi kubwa zaidi? Pengine umeona mambo fulani yenye kuwa vigumu kueleza namna yalitokea ikiwa hakuna Muumbaji, kwa mufano, maelezo ya wanasayansi yenye kuonyesha kuwa mambo yote yamepangwa muzuri sana ili kuwezesha uzima hapa duniani na mambo yenye kuhakikisha kuwa uzima haukutoka katika kitu kisichokuwa na uzima.—Soma kisanduku “ Chunguza Mambo Yenye Kuhakikisha Kama Kuna Muumbaji.”

Fikiria namna maelezo yenye kuonyeshwa hapo juu ni yenye maana. Maelezo hayo yako kama alama zenye kuonyesha mahali kwenye kuna vitu vya maana sana. Ukipata mambo yenye kusadikisha kama Mungu anakuwaka, na pia habari zenye kuaminika juu yake, utapata faida nyingi. Tuchunguze faida ine.

1.MAISHA YAKO YATAKUWA NA KUSUDI

Ikiwa maisha yana kusudi kubwa zaidi, tunataka kujua kusudi hilo ni gani na faida zenye tunaweza kupata kwa kulijua. Kwa kweli, ikiwa Mungu anakuwaka lakini hatujue hivyo, basi tunaishi bila kujua kweli ya maana zaidi katika ulimwengu.

Biblia inasema kama Mungu ndiye aliumba vitu vyote. (Ufunuo 4:11) Namna gani kujua hivyo kunaweza kufanya maisha yetu yakuwe na kusudi? Fikiria yale Biblia inafundisha juu ya jambo hilo.

Watu wako tofauti na viumbe vingine vyote duniani. Biblia inaonyesha kama Mungu alituumba kwa mufano wake, ili tuonyeshe sifa ao tabia zake. (Mwanzo 1:27) Tena, Biblia inafundisha kama watu wanaweza kuwa marafiki wa Mungu. (Yakobo 2:23) Hakuna jambo lingine linaweza kufanya maisha yetu yakuwe na kusudi zaidi isipokuwa tu kufanya urafiki pamoja na Muumbaji wetu.

Kuwa rafiki ya Mungu kuna maana gani? Marafiki wa Mungu wanaweza kuzungumuza naye moja kwa moja. Na anawaahidi kuwa atawasikiliza na kuwasaidia. (Zaburi 91:15) Kwa sababu tuko marafiki wa Mungu, tunaweza kujua mawazo yake juu ya mambo mengi. Hilo linaweza kutusaidia tuelewe muzuri majibu ya maulizo ya maana juu ya maisha yetu.

Ikiwa Mungu anakuwaka lakini hatujue hivyo, basi tunaishi bila kujua kweli ya maana zaidi katika ulimwengu

2. UTAKUWA NA AMANI YA AKILI

Kwa mufano, watu fulani wanaona kuwa ni vigumu kuamini Mungu kwa sababu wanaona mateso katika dunia. Wanauliza, ‘Sababu gani Muumbaji mwenye nguvu nyingi sana anaruhusu mateso na mambo mabaya?’

Biblia inatoa jibu lenye kufariji. Inasema kuwa Mungu hakukusudia hata kidogo watu wateseke. Wakati watu waliumbwa, maisha yao hayakukuwa na mateso. Hata katika kusudi la Mungu la mwanzoni, hakupenda watu wakufe. (Mwanzo 2:7-9, 15-17) Ni vigumu kuamini jambo hilo? Ao ni jambo la kuwazia tu? Hapana. Ikiwa kuna Muumbaji mwenye nguvu nyingi na ikiwa upendo ndio sifa yake kubwa, bila shaka hayo ndiyo maisha angekusudia watu wakuwe nayo.

Ni nini kilifikisha wanadamu katika hali ya leo? Biblia inaonyesha kuwa Mungu aliumba wanadamu wakiwa na uwezo wa kutumia uhuru wa kuchagua. Hatuko mashini, ni kusema, hatulazimishwe kumutii Mungu. Mwanaume na mwanamuke wa kwanza, waliotuzaa sisi wote, walichagua kukataa uongozi wa Mungu. Kuliko kumutii Mungu, walitafuta faida yao wenyewe kwa kuchagua njia yenye kuwapendeza. (Mwanzo 3:1-6, 22-24) Leo, tunapatwa na matokeo mabaya ya uamuzi wao.

Tunaweza kupata amani nyingi ya akili kwa kujua kama katika kusudi la Mungu, hakupenda watu wateseke. Lakini, kwa kawaida tunataka pia mateso yetu yaishe. Tuko na lazima ya tumaini la wakati unaokuja.

3. UTAKUWA NA TUMAINI

Kisha tu watu kuasi, Mungu aliahidi kama, kisha wakati fulani, atatimiza kusudi lake la mwanzoni kwa ajili ya dunia. Hakuna kitu kinaweza kumuzuia kufanya hivyo, kwa sababu yeye ni mweza-yote. (Isaya 55:11) Hivi karibuni, Mungu ataondoa matokeo yote mabaya ya uasi, na atatimiza kusudi lake la mwanzoni juu ya dunia na juu ya wanadamu.

Utapata baraka gani wakati huo? Fikiria tu ahadi mbili kati ya ahadi nyingi za Mungu kwa ajili ya wakati wetu unaokuja zinazopatikana katika Biblia.

  • AMANI ITAENEA KATIKA DUNIA YOTE NA UOVU UTAONDOLEWA. ‘Na bado muda kidogo tu, na mutu muovu hatakuwako tena; nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo. Bali wapole wataimiliki [watariti] dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.’—Zaburi 37:10, 11.

  • MAGONJWA NA KIFO HAVITAKUWA. ‘Hakuna mukaaji atakayesema: Mimi ni mugonjwa.’ (Isaya 33:24) “Yeye kwa kweli atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.”—Isaya 25:8.

Sababu gani tunaweza kuamini ahadi za Mungu zenye kupatikana katika Biblia? Kwa sababu kuna mambo yenye kuhakikisha kuwa unabii mwingi wa Biblia tayari umetimia. Lakini, tumaini la kwamba mateso yataisha wakati unaokuja halituondolee mateso ya leo. Mungu anatutolea musaada gani mwingine?

4. UTAPATA MUSAADA WA KUPAMBANA NA MAGUMU NA KUFANYA MAAMUZI YA MUZURI

Mungu anatupatia muongozo ili kutusaidia kupambana na magumu yetu na kufanya maamuzi ya muzuri. Maamuzi mengi ni madogo-madogo, lakini maamuzi mengine yanaweza kuwa na matokeo juu ya maisha yote. Hakuna mutu mwenye anaweza kututolea hekima ya muzuri kama hekima yenye Muumbaji wetu anaweza kututolea. Anaweza kujua mambo yote na ni Yeye alitupatia uzima. Kwa hiyo, anajua mambo ya muzuri kwa ajili yetu.

Biblia iko na mawazo ya Yehova Mungu, kwa sababu ni yeye aliongoza watu wenye waliiandika. Biblia inasema hivi: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.”—Isaya 48:17, 18.

Nguvu ya Mungu haina mipaka, na Mungu iko tayari kutumia nguvu yake ili kutusaidia. Biblia inaonyesha kuwa Mungu ni baba mwenye upendo anayetaka kutusaidia. Inasema hivi: ‘Baba aliye mbinguni atawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomuomba!’ (Luka 11:13) Nguvu hiyo kutoka kwa Mungu inaweza kutuongoza na kututia nguvu.

Namna gani unaweza kupata musaada huo kutoka kwa Mungu? Biblia inajibu hivi: ‘Yule anayemukaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na kwamba yeye anakuwa musawabishaji wa wale wanaomutafuta kwa bidii.’ (Waebrania 11:6) Ili usadiki kabisa kama Mungu anakuwaka, ni lazima uchunguze mwenyewe mambo yenye kuhakikisha hivyo.

UNAPENDA KUJIFUNZA MENGI ZAIDI?

Inaomba wakati ili kutafuta kweli juu ya Mungu, lakini bila shaka unaweza kupata faida kwa kufanya hivyo. Fikiria mufano wa Xiujin Xiao. Alizaliwa katika inchi ya China na anaishi sasa katika inchi ya Amerika. Anasema hivi: “Nilikuwa ninaamini fundisho la mageuzi, lakini nilipenda kujua mengi juu ya Biblia. Kwa hiyo, nilianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Katika mwaka wangu wa mwisho kwenye masomo ya juu, nilikuwa na mambo mengi ya kufanya. Kwa hiyo, sikukuwa na wakati wa kutosha ili kujifunza Biblia. Lakini sikukuwa na furaha. Wakati nilitia tena funzo langu la Biblia pa nafasi ya kwanza, nilipata furaha ya moyoni.”

Unapenda kujifunza mengi juu ya Yehova Mungu, Muumbaji wetu? Basi, tafuta wakati wa kujifunza mengi zaidi.