Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Sega la Asali

Sega la Asali

NYUKI wa asali (Apis mellifera) wanajenga sega zao kupitia nta inayofanyizwa na tezi (glandes) zinazopatikana kwenye sehemu ya ndani ya tumbo zao. Sega la asali linaonwa kuwa lilifanywa kwa ufundi wa hali ya juu sana. Sababu gani?

Fikiria hili: Ili kupata nafasi nyingi katika sehemu fulani kwa kutumia vifaa vidogo vya ujenzi, watu wenye ujuzi wa hesabu waliwazia kwa mamia ya miaka kwamba inaomba kugawanya sehemu hiyo katika umbo za pembesita kuliko kuligawanya katika umbo za pembetatu zenye pande za sawasawa ao umbo za pande ine zenye kuwa sawasawa, ao umbo lingine lolote. Lakini hawakuweza kufasiria sababu. Katika mwaka wa 1999, Profesa Thomas Hales alitoa usadikisho wa hesabu ulioonyesha faida za kile alichoita “mambo yaliyowaziwa juu ya sega la asali.” Alionyesha wazi kuwa pembesita za kawaida ndiyo njia ya muzuri ya kugawanya nafasi katika sehemu zenye kuwa sawasawa kwa kutumia vyombo vidogo vya ujenzi.

Kwa kutumia vyumba vya pembesita, nyuki wanaweza kutumia vizuri sana nafasi waliyo nayo, wanaweza kutokeza sega la asali lenye kuwa jepesi lakini ngumu kwa kutumia nta kidogo, na kuweka asali ya kutosha katika nafasi hiyo. Haishangaze kwamba sega la asali limeelezwa kuwa “ujenzi wa ufundi sana.”

Leo, wanasayansi wanaiga sega la asali la nyuki kwa kuunda majengo yenye kuwa ngumu na yenye nafasi nyingi. Kwa mufano, mafundi wa ndege (avion), wanatumia vifaa mbalimbali vyenye kuiga sega la asali ili kutengeneza ndege zenye kuwa ngumu na nyepesi na kwa hiyo zinatumia mafuta kidogo ya kuziendesha.

Unawaza namna gani? Muundo wa hali ya juu wa sega la asali ulitokana na mageuzi? Ao je, uliumbwa?