Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kuelewana

Namna ya Kuelewana

TATIZO

Wewe na bibi yako, kila mutu iko na mambo yake anayopenda juu ya kitu fulani. Kwa kweli, unaweza kuchagua jambo moja la kufanya kati ya mambo haya matatu:

  1. Unaweza kukazia mupaka mambo yafanywe vile unataka.

  2. Unaweza kukubali tu mawazo ya bibi ao bwana yako bila wewe kutaka.

  3. Ninyi wawili munaweza kuelewana.

Lakini unaweza kusema, ‘Sifurahie wazo la kuelewana. Ni kama vile hakuna mumoja kati yetu atapata mambo tunayotaka!’

Uwe hakika kama kuelewana hakutawafanya ninyi wawili mukose furaha, ikiwa tu munafanya hivyo muzuri. Lakini mbele ya kuzungumuzia namna ya kuelewana, kuna mambo machache unapaswa kujua juu ya ufundi huo wa maana.

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Ili kuelewana, inaomba kutumika pamoja. Mbele ya kufunga ndoa, inawezekana ulizoea kufanya maamuzi yako mwenyewe. Sasa mambo yamebadilika, na ninyi wawili munapaswa kufanya ndoa yenu kuwa ya maana zaidi kuliko mambo kila mutu anapenda. Kuliko kuwazia hilo kuwa kizuizi, ufikirie faida za kufanya hivyo. Mwanamuke mumoja anayeitwa Alexandra anasema hivi: “Mawazo ya watu wawili yakichangwa pamoja, hilo linaweza kusaidia kupata njia muzuri zaidi ya kumaliza tatizo kuliko ile mutu anaweza kupata yeye mwenyewe.”

Ili kuelewana, inaomba kuwa na mawazo mazuri. John Gottman, mushauri wa ndoa anasema hivi: “Haiko lazima ukubaliane na kila jambo bibi ao bwana yako anasema ao kuamini, lakini unapaswa kuwa tayari kufikiria mawazo yake. Ikiwa unakaa ukiwa mwenye kupachika (kukunja) mikono yako na kukataa kwa kutikisa kichwa chako (ao kukataa tu ndani ya moyo) wakati bibi ao bwana yako anajaribu kuzungumuza na wewe juu ya tatizo fulani, mazungumuzo yenu hayatawafikisha nafasi yoyote.” *

Ili kuelewana, inaomba kujinyima. Hakuna mutu anafurahia kuishi na bibi ao bwana anayeamini kuwa mawazo yake ndiyo ya muzuri zaidi. Ni muzuri zaidi wakati bibi na bwana wote wawili wana roho ya kujinyima. Mwanamuke mumoja anayeitwa June anasema hivi: “Kuna wakati ninakubaliana na bwana yangu ili tu nimufurahishe, lakini wakati fulani yeye pia ananifanyia hivyo. Ni hivyo ndoa inapaswa kuwa—kutoa na kupokea, wala si kupokea tu.”

 MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Uanze sasa. Mara nyingi sauti unayoanza nayo mazungumuzo ndiyo unamaliza nayo. Ikiwa unaanza na maneno makali, ni vigumu sana kufikia kuelewana kwa amani. Kwa hiyo, ufuate shauri hili la Biblia: ‘Mujivike [muvae] huruma, fazili, unyenyekevu wa akili, upole, na ustahimilivu.’ (Wakolosai 3:12) Sifa kama hizo zitakusaidia wewe na bibi ao bwana yako kuepuka mabishano na kutafuta namna ya kumaliza tatizo.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 4:6.

Utafute mambo munayokubaliana. Ikiwa munajaribu kuelewana lakini munafikia katika mabishano makali, inaweza kuwa ni kwa sababu wewe na bibi ao bwana yako munakazia sana mawazo ambayo hamukubaliane. Kuliko kufanya hivyo, muone ni wapi munakubaliana. Ili kukusaidia uone mambo munakubaliana, jaribu kufanya hivi:

Kila mumoja wenu achukue karatasi na aigawanye katika sehemu mbili. Katika sehemu ya kwanza, uandike ni mambo gani unashikilia zaidi juu ya hali hiyo. Katika sehemu ya pili, uandike mambo unaona kuwa munaweza kuelewana. Kisha muzungumuzie pamoja mambo yote muliandika. Munaweza kuona kuwa munakubaliana katika mambo mengi kuliko namna muliwazia. Ikiwa ni vile, haitakuwa vigumu sana kuelewana. Hata ikiwa hamukubaliane katika mambo mengi, kuwa na mambo yote juu ya tatizo hilo yakiwa yenye kuandikwa kwenye karatasi kutakusaidia wewe na bibi ao bwana yako kuona tatizo hilo kwa njia iliyo wazi zaidi.

Muchange mawazo ili kumaliza matatizo. Matatizo fulani yanaweza kuwa mepesi kumaliza. Lakini, kuhusu matatizo magumu sana, bibi na bwana wanaweza kukaza muungano wao wa ndoa kwa kuchanga mawazo na kupata njia ya kumaliza tatizo yenye pengine kila mumoja hangeweza kupata yeye mwenyewe.—Kanuni ya Biblia: Mhubiri 4:9.

Uwe tayari kubadilisha mawazo yako. Biblia inasema hivi: ‘Kila mutu mumoja-mumoja kati yenu na amupende hivyo muke [bibi] wake kama vile anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, muke anapaswa kumuheshimu sana mume [bwana] wake.’ (Waefeso 5:33) Wakati bibi na bwana wote wawili wanajisikia kuwa wanapendana na wanaheshimiana, kila mumoja atakuwa tayari kufikiria mawazo ya mwengine, na hata kubadilisha mawazo yake. Bwana mumoja anayeitwa Cameron anasema hivi: “Kuna mambo labda haungependa kufanya, lakini kwa sababu ya kuchochewa na bibi ao bwana yako, unafikia kuyapenda.”—Kanuni ya Biblia: Mwanzo 2:18.

^ fu. 12 Maneno hayo yametoka katika kitabu The Seven Principles for Making Marriage Work.