Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Kiungo cha Kuogelea cha Nyangumi Mwenye Sehemu ya Mugongo Yenye Kuinuka

Kiungo cha Kuogelea cha Nyangumi Mwenye Sehemu ya Mugongo Yenye Kuinuka

NYANGUMI mwenye kukomaa mwenye sehemu ya mugongo yenye kuinuka ni mukubwa zaidi na muzito zaidi kuliko motokari ya kubeba watu. Hata hivyo, munyama huyo mukubwa zaidi wa baharini ni mwepesi kiajabu wakati anaingia na kugeuka ndani ya bahari. Namna gani munyama huyo mukubwa anaweza kuwa mwepesi hivyo? Siri ya wepesi wake inapatikana katika sehemu zenye kuinuka-inuka zilizo kwenye viungo vyake vya kuogelea.

Fikiria jambo hili: Nyangumi wengi na wanyama wengine wa baharini wana viungo vya kuogelea vyenye sehemu za mwisho zilizo laini. Lakini, nyangumi mwenye sehemu ya mugongo yenye kuinuka iko tofauti. Ana sehemu zenye kuinuka​-inuka kabisa kwenye mwisho wa viungo vyake vya kuogelea. Wakati nyangumi huyo anaogelea, maji yanatiririka juu ya sehemu hizo zenye kuinuka-inuka na kufanyiza mawimbi mengi ya maji. Wakati nyangumi anaposonga mbele, sehemu hizo zinafanyiza nyuma yake njia ya maji yanayotiririka na kutokeza musukosuko mukubwa ndani ya bahari. Sehemu hizo zenye kuinuka​-inuka zinapopasua maji zinamupatia nguvu za kunyanyuka, na hilo linamuwezesha kuinua viungo vyake vya kuogelea kwenye umbali fulani juu ya maji kuelekea juu huku akiendelea na mwendo wake. Pia akiwa mwenye kuinuka juu zaidi, sehemu hizo zenye kuinuka-inuka za viungo vyake vya kuogelea zinamuwezesha kusonga kwa urahisi zaidi bila kuzuiliwa na maji—hiyo ndiyo faida moja ya maana zaidi ya viungo hivyo virefu vya kuogelea vya nyangumi huyo, kila kimoja cha viungo hivyo kina urefu wa sehemu moja ya tatu ya mwili wake wote.

Wachunguzi wanafuata kanuni hiyo ili kutengeneza sukani za mashua, majembe ya mashua ya kupasua maji, vinu ao visagio vinavyoendeshwa kwa upepo, majembe ao mabawa ya helikopta ambayo yanafanya kazi vizuri zaidi.

Unawaza namna gani? Je, kiungo hicho cha kuogelea cha nyangumi mwenye sehemu ya mugongo yenye kuinuka kilijifanya chenyewe? Ao ni kazi ya uumbaji?