Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Chembe ya chachu ni ya ajabu kabisa. Iko na kiini (noyau) yenye kupangwa muzuri kabisa, yenye ndani yake muko ADN. Na iko na vitu vyenye kuwa sawa mashine za kidogo-kidogo sana zenye zinapanga, zinasafirisha na kubadilisha mamolekile. Ile mambo yote ni ya maana juu chachu iendelee kuishi.

Vitu vyenye Uzima Vinaonyesha Nini?

Vitu vyenye Uzima Vinaonyesha Nini?

Vitu vyenye uzima vyenye kutuzunguka vinakomalaka, vinatembeaka na vinazalanaka. Vinafanya dunia ikuwe yenye kupendeza sana tofauti na sayari zingine. Na leo, watu wanajua mambo mingi sana kuliko zamani. Vitu vyenye uzima vinaonyesha kama kuko mwenye aliviumba ao vilijitokea? Fikiria mawazo yenye kufuata.

Namna vitu vyenye uzima viko inaonyesha kama vilifanywa. Vitu vyenye uzima vinafanyizwa na sehemu za kidogo-kidogo zenye kuitwa chembe. Tunaweza kufananisha chembe na izine za kidogo-kidogo zenye kufanya kazi mingi ya ajabu juu vitu vyenye uzima viendelee kuishi na vizalane. Hata vitu vyenye uzima vya kidogo sana vinatumika mu njia ya ajabu kabisa. Kwa mufano, fikiria chachu yenye inatumiwaka juu ya kutengeneza mikate. Chachu ni kiumbe yenye kuwa na chembe moja tu. Tukiilinganisha na chembe ya mwanadamu, chembe ya chachu inaweza kuonekana kuwa haiko ya ajabu. Hata vile, ile chembe ni ya ajabu kabisa. Chembe za chachu ziko na kiini (noyau) yenye kupangwa muzuri kabisa, yenye ndani yake muko ADN. Zile chembe ziko na vitu vyenye kuwa sawa mashine za kidogo-kidogo sana zenye zinapanga, zinasafirisha na kubadilisha mamolekile. Ile mambo yote ni ya maana juu chachu ziendelee kuishi. Wakati chembe ya chachu inakosa chakula, inaachaka kufanya kazi na inabakia tu sawa yenye inalala. Njo maana chachu inaweza kuwekwa wakati murefu mu mafiga bila kufa. Na wakati itaomba kuitumikisha, itakuwa ingali natumika muzuri.

Kwa miaka mingi wanasayansi wamejifunza chembe za chachu, juu waweze kuelewa muzuri chembe za mwanadamu. Hata vile, wangali na mambo mingi ya kujifunza. Ross King, profesa ku Masomo ya Juu ya Teknolojia mu Suède, anasema hivi: “Hata watu wenye kujifunza mambo ya biolojia wakutane wote juu ya kuchunguza kitu yenye uzima yenye inaonekana kuwa yenye haiko ya ajabu, sawa vile chachu, hawawezi kuielewa muzuri.”

Unawaza namna gani? Chembe ya chachu, yenye iko ya ajabu na yenye watu wameshindwa kuelewa muzuri kabisa, ilijitokeza yenyewe ao kuko mwenye aliifanya?

Kitu yenye uzima inatokanaka tu na kitu ingine yenye uzima. Molekile zenye kuitwa nikleotide njo zinafanyizaka ADN. Kila chembe ya mwanadamu iko na nikleotide miliare 3.2. Zile nikleotide ni zenye kupangwa kwa utaratibu kabisa juu chembe iweze kutokeza anzime na proteine.

Wanasayansi wanasema kama ikiwa nikleotide zinajaribu kujikutanisha pamoja kwa bahati mara mamiliare na mamiliare, ni mara moja tu njo zinaweza kufanikiwa kujipanga kwa utaratibu wenye unawezesha chembe itokeze anzime na proteine. Kusema kweli ile ni jambo yenye haiwezekane kabisa.

Wanasayansi wameshindwa kuonyesha kama uzima unaweza kutokea ku vitu vyenye havina uzima.

Mwanadamu iko tofauti na viumbe vingine. Siye wanadamu tuko na uwezo mbalimbali wenye unafanya tufurahie kabisa maisha kuliko viumbe vingine. Tuko na uwezo wa hali ya juu wa kutengeneza vitu, tunaweza kujifunza kuishi muzuri na wengine, na tuko na uwezo wa kuonyesha namna tunajisikia. Tunaweza kufurahia kabisa onjo, harufu, sauti, rangi, na kuona mambo mbalimbali. Tunaweza kupanga mambo yenye tutafanya mu siku zenye ziko nakuya na tunaweza kutafuta kujua juu ya nini tuko naishi.

Unawaza namna gani? Tuko na ile uwezo mbalimbali ni juu tukiikosa tutashindwa kuishi na kuzalana? Ao ile uwezo mbalimbali inaonyesha kama uzima ni zawadi yenye Muumbaji mwenye upendo ametupatia?