Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Juu ya Nini Tunatesekaka, Tunazeekaka, na Kufa?

Juu ya Nini Tunatesekaka, Tunazeekaka, na Kufa?

Muumbaji wetu anatuonaka sawa vile watoto wake. Kwa hiyo, hapendake tuteseke. Lakini hata vile, leo mateso iko mingi sana. Juu ya nini?

Tunatesekaka Juu ya Wazazi Wetu wa Kwanza

“Kupitia mutu mumoja, zambi iliingia katika ulimwengu, na kifo kupitia zambi na ni vile kifo kilienea kwa watu wote.”​—WAROMA 5:12.

Wakati Mungu aliumba wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Eva, aliwapatia miili na akili yenye kuwa kamilifu. Aliwatia katika paradiso ku dunia, mu bustani ya muzuri yenye kuitwa bustani ya Edeni. Aliwaambia wakule matunda ya miti yote ya mu ile bustani, lakini aliwakataza tu matunda ya muti moja. Adamu na Eva walichagula kukula matunda ya ile muti yenye Mungu aliwakataza, na ile ilikuwa zambi. (Mwanzo 2:15-17; 3:1-19) Kisha wao kumukosea Mungu, aliwafukuza mu ile bustani, na wakaanza maisha ya nguvu sana. Kisha wakati fulani, wakazala watoto, na wale watoto nao wakakuwa na maisha ya nguvu. Wote walianza kuzeeka na kufa. (Mwanzo 3:23; 5:5) Juu siye wote tuko watoto wa Adamu na Eva, njo maana tunagonjwaka, tunazeekaka na kufa.

Tunatesekaka Juu ya Roho Waovu

“Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.”​—1 YOHANA 5:19.

Ule “muovu” ni Shetani. Ni malaika mwenye alimuasi Mungu. (Yohana 8:44; Ufunuo 12:9) Kisha, malaika wengine wakajiunga na Shetani. Wanaitwa pepo wachafu. Wale malaika wabaya wanatumia nguvu yao, juu ya kudanganya watu wasimutii Muumbaji. Wanachochea watu wengi wafanye mambo ya mubaya. (Zaburi 106:35-38; 1 Timoteo 4:1) Shetani na pepo wachafu, wanapendaka kufanya maisha ya watu ikuwe nguvu na wanakuwaka wanafurahi wakati watu wanateseka.

Wakati Fulani Tunatesekaka Juu ya Kukamata Maamuzi ya Mubaya

“Kitu chochote chenye mutu anapanda, ni kile atavuna pia.”​—WAGALATIA 6:7.

Mu njia mbalimbali, siye wote tunatesekaka juu ya zambi yenye tuliriti na juu ya mambo yenye Shetani iko nachochea watu wa hii dunia wafanye. Lakini wakati fulani, watu wao wenyewe njo wanajileteaka magumu mu maisha. Namna gani? Wakati wanafanya mambo ya mubaya ao wanakamata maamuzi ya mubaya, mara mingi wanavunaka tu mambo ya mubaya. Lakini wakati watu wanafanya mambo ya muzuri, wanavunaka tu mambo ya muzuri. Kwa mufano, bwana ao baba mwenye kuwa muaminifu, mwenye anatumikaka nguvu, na kupenda familia yake, atavuna mambo ya mingi ya muzuri na familia yake itakuwa na furaha. Lakini baba mwenye anapendaka michezo ya makuta, mwenye anakunywaka pombe sana, ao muvivu, anaweza kufanya familia yake ikuwe maskini. Kwa hiyo, ni jambo ya hekima tumusikilize Muumbaji wetu. Anapenda tuvune mambo ya mingi ya muzuri, kutia ndani ‘amani ya mingi.’​—Zaburi 119:165.

Tunaishi mu “Siku za Mwisho”

“Katika siku za mwisho . . . , watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, . . . wenye hawatii wazazi, . . . wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema.”​—2 TIMOTEO 3:1-5.

Leo, watu wengi wako na tabia za vile. Ile inaonyesha kabisa kama tunaishi mu “siku za mwisho” za hii ulimwengu. Tena, maandiko ilionyesha mbele ya wakati kama, tutajua kama tunaishi mu siku za mwisho wakati tutaona upungufu wa chakula, matetemeko makubwa ya inchi, na magonjwa. (Matayo 24:3, 7, 8; Luka 21:10, 11) Ile inafanya kukuwe mateso ya mingi na kifo.