Ona video zinazopatikana

Utangulizi wa Vitabu vya Biblia

Video hizi za mufupi zinatupatia habari zenye kuwa mu kitabu fulani cha Biblia na juu ya wakati kiliandikwa. Tumia mafundisho yenye kuwa mu video juu ufanye usomaji wako wa Biblia ukuwe muzuri zaidi.

Utangulizi wa Biblia

Ona namna vitabu vyote vya Biblia vinazungumuzia habari ya maana sana ya Biblia, ni kusema namna Ufalme wa Yesu Kristo utatakasa jina ya Yehova.

Utangulizi wa Kitabu cha Mwanzo

Kitabu cha Mwanzo kinatupatia habari ya maana juu ya namna wanadamu walianza na namna mateso na kifo vilianza.

Utangulizi wa Kitabu cha Kutoka

Mungu alikomboa Waisraeli mu utumwa wa Misri na kuwafanya kuwa taifa yake.

Utangulizi wa Kitabu cha Mambo ya Walawi

Ona namna kitabu cha Mambo ya Walawi kinafasiria utakatifu wa Mungu na juu ya nini ni lazima tukuwe watakatifu.

Utangulizi wa Kitabu cha Hesabu

Ona juu ya nini ni jambo ya lazima kumutii Yehova na kuheshimia watu wenye anatumia ili kuongoza watu wake.

Utangulizi wa Kitabu cha Hesabu

Ona juu ya nini ni jambo ya lazima kumutii Yehova na kuheshimia watu wenye anatumia ili kuongoza watu wake.

Utangulizi wa Kitabu cha Kumbukumbu la Torati

Ona namna Sheria yenye Yehova alipatia Israeli inaonyesha kama alipenda sana watu wake.

Utangulizi wa Kitabu cha Yoshua

Ona namna Waisraeli walipata ushindi na namna wanagawanya inchi yenye Mungu aliwapatia.

Utangulizi wa Kitabu cha Waamuzi

Hii kitabu yenye kuwa na habari yenye inatia moyo sana, ilipewa jina ya wanaume hodari wenye Mungu alitumia juu ya kukomboa watu wake kutokana na watu wabaya.

Utangulizi wa Kitabu cha Rutu

Hii kitabu inazungumuzia upendo wa kujitoa wenye kijana moya mwanamuke mujane alionyesha mama-mukwe wake mujane, na inazungumuzia pia namna Yehova aliwapatia zawabu.

Utangulizi wa Kitabu cha 1 Samweli

Ona namna historia ya Waisraeli inatoka mu wakati wa waamuzi na kufika mu wakati wenye wafalme walianza kutawala.

Utangulizi wa Kitabu ya 2 Samweli

Ona namna unyenyekevu na imani ya Daudi vilifanya akuwe kati ya watu wenye kupendwa na kujulikana zaidi wenye kutajwa mu Biblia.

Utangulizi wa Kitabu ya 1 Wafalme

Ona historia wa Waisraeli kuanzia wakati wa utawala wenye utukufu na wenye kuendelea muzuri wa Sulemani mupaka wakati wa muvurugo wa falme mbili, ufalme wa Israeli na wa Yuda.

Utangulizi wa Kitabu ya 2 Wafalme

Ona namna uasi imani unaharibu ufalme wa kaskazini wa Israeli wakati ule ule Yehova anabariki wachahe wenye wanaendelea kumuabudu kwa moyo wote.

Utangulizi wa Kitabu ya 1 Mambo ya Nyakati

Ona historia na maisha yenye kufurahisha ya Daudi, mufalme mwenye kumuogopa Mungu, kuanzia wakati aliwekwa kuwa mufalme mupaka kifo yake.

Utangulizi wa Kitabu cha Ezra

Yehova anatimiza ahadi zake za kukomboa watu wake kutoka katika utumwa wa Babiloni na kurudisha ibada safi katika Yerusalemu.

Utangulizi wa Kitabu cha Nehemia

Kitabu cha Biblia cha Nehemia kiko na mafundisho mengi ya muzuri kwa ajili ya waabudu wote wa kweli wa leo.

Utangulizi wa Kitabu cha Esta

Mambo yenye ilitokea katika siku za Esta, itafanya ukuwe na imani yenye nguvu, na itakusaidia ujue kama Yehova Mungu ana uwezo wa kukomboa watu wake wakati wa majaribu leo.

Utangulizi wa Kitabu cha Ayubu

|Watu wote wenye kumupenda Yehova watajaribiwa. Habari ya Ayubu inatuhakikishia kama inawezekana tuendelee kuwa washikamanifu na kuunga mukono haki ya Yehova ya kutawala.

Utangulizi wa Kitabu cha Zaburi

Kitabu cha Zaburi kinaunga mukono haki ya Yehova ya kutawala, kinasaidia watu wenye wanamupenda na kuwatuliza, na kinaonyesha namna Ufalme wake utabadilisha ulimwengu.

Utangulizi wa Kitabu cha Methali

Pata muongozo wa Mungu juu ya kila sehemu ya maisha yetu, kama vile mambo ya biashara na mambo ya familia.

Utangulizi wa Kitabu cha Mhubiri

Mufalme Sulemani anazungumuzia mambo ya maana kabisa katika maisha na anaonyesha pia mambo yenye kupingana na hekima ya Mungu.

Utangulizi wa Wimbo wa Sulemani

Upendo wa kweli kati ya mwanamuke Mushulami na kijana muchungaji unaitwa “mwali wa moto wa Yah.” Sababu gani?

Utangulizi wa Kitabu cha Isaya

Kitabu cha Isaya ni kitabu cha unabii wa kweli kabisa wenye unaweza kutia nguvu tumaini lako katika Yehova, Mutimizaji wa ahadi na Mungu wa wokovu wetu.

Utangulizi wa Kitabu cha Yeremia

Yeremia alitimiza kwa uaminifu mugao wake, hata kama alipata matatizo. Fikiria namna mufano wake unaweza kusaidia Wakristo leo.

Utangulizi wa Kitabu cha Maombolezo

Kitabu cha Maombolezo kiliandikwa na nabii Yeremia na kinazungumuzia namna watu walihuzunika juu ya kuharibiwa kwa Yerusalemu na kinaonyesha namna Mungu anasamehe wenye wanatubu

Utangulizi wa Kitabu cha Ezekieli

Ezekieli alitimiza kwa unyenyekevu na bila kuogopa mugawo wowote wenye Mungu alimupatia, hata kama ulikuwa nguvu. Mufano wake ni wa maana sana kwetu leo.

Utangulizi wa Kitabu cha Danieli

Danieli na wenzake watatu walibakia waaminifu kwa Yehova wakati wa magumu. Mufano wao, na kutimizwa kwa unabii kunaweza kutuletea faida sasa, wakati huu wa mwisho.

Utangulizi wa Kitabu cha Hosea

Unabii wa hosea uko na mafundisho ya maana kwetu leo kuhusu namna Yehova anasamehe watenda-zambi wenye wanatubu na aina ya ibada yenye anakubali.

Utangulizi wa Kitabu cha Yoeli

Yoeli alitoa unabii kuhusu “siku ya Yehova” yenye kukaribia sana na alionyesha namna ya kuokoka. Leo, unabii huo ni wa maana tena zaidi.

Utangulizi wa Kitabu cha Amosi

Yehova alitumia mwanaume huyo wa hali ya chini ili kufanya kazi kubwa. Mufano wa Amosi unaweza kutufundisha somo gani za lazima?

Utangulizi wa Kitabu cha Obadia

Ndio kitabu kifupi sana katika Maandiko ya Kiebrania. Unabii wa Obadia unatoa tumaini na unaahidi kutetewa kwa utawala wa Yehova.

Utangulizi wa Kitabu cha Yona

Nabii Yona alikubali kurekebishwa, alitimiza mugao wake, na alijifunza somo kubwa juu ya upendo mushikamanifu wa Mungu na rehema. Habari yake itagusa kabisa moyo wako.

Utangulizi wa Kitabu cha Mika

Unabii huu wenye uliongozwa na roho ya Mungu unaweza kutia nguvu imani yetu kwamba Yehova anatuomba tu mambo yenye tunaweza kufanya na kwa faida yetu.

Utangulizi wa Kitabu cha Nahumu

Unabii wa Nahumu unatutolea tumaini kama Yehova hakose kutimiza neno lake na kama anabariki wale wanatumainia Ufalme wake ili kupata amani na wokovu.

Utangulizi wa Kitabu cha Habakuki

Tunaweza kuwa hakika kama sikuzote Yehova anajua wakati wenye kufaa na namna yenye kufaa ya kuokoa watu wake.

Utangulizi wa Kitabu cha Sefania

Sababu gani tunapaswa kuepuka kuwaza kama siku ya Yehova ya hukumu haitakuja?

Utangulizi wa Kitabu cha Hagai

Unabii wa Hagai unakazia kama tunapaswa kuhangaikia kwanza ibada ya Mungu kuliko kuhangaikia kwanza faida zetu.

Utangulizi wa Kitabu cha Zekaria

Maono na unabii mbalimbali wenye kuongozwa na roho ulitia nguvu watu wa Mungu wa zamani. Unabii huo-huo unatuhakikishia kama Yehova anaendelea kututegemeza leo.

Utangulizi wa Kitabu cha Malaki

Ni unabii kuhusu kanuni za Yehova zenye hazibadilike, rehema yake, na upendo wake. Unabii huo unatutolea pia somo za maana sana kuhusu hali zenye tunapambana nazo leo.

Utangulizi wa Kitabu cha Mathayo

Ufurahie kujifunza mambo makubwa juu ya kitabu hicho cha Biblia, kitabu cha kwanza kati ya vitabu ine vya Injili.

Utangulizi wa Kitabu cha Luka

Ni habari gani zinapatikana tu katika Injili ya Luka?

Utangulizi wa Kitabu cha Yohana

Injili ya Yohana inakazia upendo wa Yesu kwa wanadamu, mufano wake wa unyenyekevu, na kama yeye ni Masiya, Mufalme wa Ufalme wa Mungu.

Utangulizi wa Kitabu cha Matendo ya Mitume

Wakristo wa kwanza-kwanza walihubiri kwa bidii ili kufanya wanafunzi kutoka watu wa mataifa yote. Kitabu cha Matendo kinaweza kuchochea bidii yako na kuongeza furaha yako kwa ajili ya kazi ya kuhubiri.

Utangulizi wa kitabu cha Waroma

Kiliongozwa na roho ili kuonyesha kama Yehova hana ubaguzi na kama ni lazima kuamini Yesu Kristo.

Utangulizi wa Kitabu cha 1 Wakorinto

Hii barua ya Paulo iko na mashauri yenye iliongozwa na roho. Inazungumuzia umoja, mwenendo muzuri, upendo, na imani katika ufufuo.

Utangulizi wa Kitabu cha 2 Wakorinto

Yehova, “Mungu wa faraja yote,” anapatia nguvu na kutegemeza watumishi wake.

Utangulizi wa Kitabu cha Wagalatia

Barua ya Paulo kwa Wagalatia iko na faida pia kwetu leo sawa vile tu ilikuwaka wakati iliandikwa. Inaweza kusaidia Wakristo wote wa kweli waendelee kuwa waaminifu.

Utangulizi wa Kitabu cha Waefeso

Hii barua yenye kuongozwa na roho inakazia kusudi la Mungu la kuleta amani na umoja kupitia Yesu Kristo.

Utangulizi wa Kitabu cha Wafilipi

Kama unavumilia majaribu unaweza kutia wengine moyo wasiogope.

Utangulizi wa Kitabu cha Wakolosai

Tunaweza kumufurahisha Yehova kwa kutumikisha mambo yenye tunajifunza, kwa kuwa tayari kusamehe wengine, na kwa kutambua cheo cha Yesu na mamlaka yake.

Utangulizi wa Kitabu cha 1 Watesalonike

Tunapaswa kuwa macho kiroho, ‘kuchunguza mambo yote,’ ‘kusali bila kuacha,’ na kutiana moyo.

Utangulizi wa Kitabu cha 2 Watesalonike

Paulo anarekebisha mawazo yenye kuwa na makosa juu ya kuja kwa siku ya Yehova, na anatia moyo ndugu waendelee kuwa na imani yenye nguvu.

Utangulizi wa Kitabu cha 1 Timoteo

Paulo aliandika barua ya Kwanza kwa Timoteo ili kuonyesha utaratibu wa tengenezo katika kutaniko na kuonya juu ya mafundisho ya uongo na kupenda feza.

Utangulizi wa Kitabu cha 2 Timoteo

Paulo anatia moyo Timoteo atimize utumishi wake kwa ukamili.

Utangulizi wa Kitabu cha Tito

Barua ya Paulo kwa Tito inazungumuzia matatizo yenye ilikuwa mu makutaniko ya kule Krete, na inaonyesha mambo yenye inaombwa ili kuwa muzee

Utangulizi wa Kitabu cha Filemoni

Hii ni barua ya mufupi, lakini yenye kufundisha sifa fulani za lazima kama vile unyenyekevu, wema, na kusamehe.

Utangulizi wa Kitabu cha Waebrania

Ibada ya Kikristo inategemea mambo ya muzuri zaidi kuliko hekalu yenye kuonekana na zabihu za wanyama.

Utangulizi wa Kitabu cha Yakobo

Yakobo anatumia mifano yenye kuwa wazi ili kufundisha kanuni za maana za Kikristo.

Utangulizi wa Kitabu cha Petro wa Kwanza

Katika barua yake ya kwanza, Petro anatutia moyo tuendelee kufanya kazi na kumutupia Mungu mahangaiko yetu yote.

Utangulizi wa Kitabu cha Petro wa Pili

Barua ya pili ya Petro inatutia moyo tukuwe waaminifu wakati tuko tunangojea mbingu mupya na dunia mupya.

Utangulizi wa Kitabu cha 1 Yohana

Barua ya Yohana inatoa angalisho juu ya mupinga-kristo na inatusaidia kuona mambo yenye tunapaswa kupenda na yenye tunapaswa kuchukia.

Utangulizi wa Kitabu cha 2 Yohana

Barua ya Yohana inatukumbusha kama tuendelee kutembea katika kweli na tujilinde kutokana na wadanganyifu.

Utangulizi wa Kitabu cha 3 Yohana

Barua ya tatu ya Yohana inafundisha somo la muzuri sana la kukaribisha wageni.

Utangulizi wa Kitabu cha Yuda

Yuda anaonyesha wazi njia za uongo za wale wenye wanajaribu kudanganya na kupotosha Wakristo.

Utangulizi wa Kitabu cha Ufunuo

Maono yenye kuchochea sana yenye kuwa katika kitabu cha Ufunuo inaonyesha namna Ufalme wa Mungu utatimiza mapenzi yake kwa ajili ya wanadamu na dunia.

Ona pia...