Ona video zinazopatikana

Mungu Iko na Majina Ngapi?

Mungu Iko na Majina Ngapi?

Jibu la Biblia

 Mungu iko na jina moja tu la pekee. Katika Kiebrania linaandikwa יהוה na mara nyingi linaandikwa “Yehova” katika Kiswahili. * Kupitia nabii wake Isaya, Mungu alisema hivi: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.” (Isaya 42:8) Jina hilo linapatikana mara 7 000 hivi katika maandishi ya zamani ya Biblia. Jina hilo linarudiliwa mara nyingi zaidi kuliko neno lingine lolote lenye kuhusiana na Mungu, na mara nyingi sana kuliko jina lingine la pekee. *

Yehova iko na majina mengine?

 Hata kama Biblia inataja Mungu katika jina lake la pekee, inatumia pia majina mengi ya cheo kumuhusu. Liste yenye kufuata ya majina ya cheo inaonyesha namna kila jina linafunua jambo fulani kuhusu utu wa Yehova.

Jina la cheo

Andiko

Maana

Allah

(Hakuna andiko)

Linatoka katika Kiarabu. Neno “Allah” haiko jina la pekee, lakini ni jina la cheo lenye kumaanisha “Mungu.” Tafsiri za Biblia katika Kiarabu na luga zingine zinatumia “Allah” pa nafasi ya “Mungu.”

Mweza-Yote

Mwanzo 17:1

Iko na nguvu ya ajabu. Maneno ya Kiebrania ʼEl Shad·daiʹ, “Mungu Mweza-Yote,” yanapatikana mara saba katika Biblia.

Alfa na Omega

Ufunuo 1:8; 21:6; 22:13

“Wa kwanza na wa mwisho,” ao “mwanzo na mwisho.” Hilo linamaanisha kwamba hakukuwa Mungu Mweza-Yote mbele ya Yehova na hakutakuwa mwingine kisha yeye. (Isaya 43:10) Alfa na omega ni herufi ya kwanza na ya mwisho ya alfabeti ya Kigiriki.

Muzee wa Siku

Danieli 7:​9, 13, 22

Hana mwanzo; iko milele mbele ya mutu yeyote ao kitu chochote kuwa.​—Zaburi 90:2.

Muumba

Isaya 40:28

Aliumba kila kitu.

Baba

Mathayo 6:9

Mupaji wa uzima.

Mungu

Mwanzo 1:1

Mwenye kustahili kutolewa ibada; Mwenye kuwa na nguvu. Neno la Kiebrania ʼElo·himʹ linatumiwa kwa uwingi ili kuonyesha ukuu, heshima na utukufu wa Yehova.

Mungu wa miungu

Kumbukumbu la Torati 10:17

Mungu mukuu mwenye kuwa tofauti na ‘miungu isiyo na samani’ yenye kuabudiwa na watu fulani.​—Isaya 2:8.

Mufundishaji Mukuu

Isaya 30:20, 21

Anatoa mafundisho na muongozo wenye faida.​—Isaya 48:17, 18.

Mutengenezaji Mukuu

Zaburi 149:2

Aliumba vitu vyote.​—Ufunuo 4:​11.

Mungu mwenye furaha

1 Timotheo 1:​11

Anajulikana kuwa mwenye furaha na shangwe.​—Zaburi 104:31.

Musikiaji wa sala

Zaburi 65:2

Anasikiliza yeye mwenyewe kila sala yenye kutolewa kwake katika imani.

Mimi Niko Ambaye Niko

Kutoka 3:​14, Union Version

Anakuwa chochote anataka ili kutimiza kusudi lake. Maneno hayo yametafsiriwa pia “Mimi Ndimi Niliye” ao “Nitakuwa Kile Nitakachokuwa.” (Biblia Habari Njema; Tafsiri ya Ulimwengu Mpya) Majina hayo yanasaidia kufasiria maana ya jina la Mungu, Yehova, lenye kutajwa katika mustari wenye kufuata.​—Kutoka 3:​15.

Mwenye Wivu

Kutoka 34:14, Biblia Habari Njema

Havumilie ushindani wowote katika ibada.

Mufalme wa umilele

Ufunuo 15:3

Utawala wake hauna mwanzo wala mwisho.

Bwana

Zaburi 135:5

Mumiliki; Kiebrania ʼA·dhohnʹ na ʼAdho·nimʹ.

Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Bwana wa majeshi

Isaya 1:9, Biblia Habari Njema; Waroma 9:​​29, Biblia Habari Njema

Anaongoza majeshi mengi sana ya malaika. Jina hilo la cheo linaweza pia kutafsiriwa “Yehova wa majeshi.”—Waroma 9:​29, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

Aliye Juu Zaidi

Zaburi 47:2

Iko na cheo cha juu zaidi.

Mutakatifu Zaidi

Methali 9:​10

Ni mutakatifu (safi kabisa) kuliko kiumbe chochote.

Mufinyazi

Isaya 64:8

Iko na mamlaka juu ya kila mutu mumoja-mumoja na mataifa, kama vile mufinyanzi iko na mamlaka juu ya udongo.​—Waroma 9:​20, 21.

Mukombozi

Isaya 41:14

Anakomboa na kununua wanadamu kutoka katika zambi na kifo kupitia zabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo.​—Yohana 3:​16.

Mwamba

Zaburi 18:​2, 46

Kimbilio salama na chanzo cha wokovu.

Mwokozi

Isaya 45:21

Anaokoa wakati wa hatari ao wa maangamizi.

Muchungaji

Zaburi 23:1

Anatunza waabudu wake.

Bwana Mwenye Enzi Kuu

Mwanzo 15:2

Iko na mamlaka makubwa zaidi; Kiebrania ʼAdho·naiʹ.

Aliye Mukuu Zaidi

Daniel 7:​18, 27

Mwenye kuwa na mamlaka ya juu zaidi.

Majina ya mahali katika Maandiko ya Kiebrania

 Katika Biblia, majina fulani ya mahali yanatia ndani jina la Mungu la pekee, lakini hayako majina mengine ya Mungu.

Jina la mahali

Andiko

Maana

Yehova-yire

Mwanzo 22:13, 14

“Yehova Ataandaa.”

Yehova-nisi

Kutoka 17:15

“Mwenyezi-Mungu ni Bendera Yangu.” (Biblia Habari Njema) Yehova ni Mungu mwenye watu wake wanaweza kumuendea ili kupata ulinzi na musaada.​—Kutoka 17:13-​16.

Yehova-shalomu

Waamuzi 6:​23, 24

“Yehova Ni Amani.”

Yehova-shama

Ezekieli 48:35

“Yehova Mwenyewe Iko Hapo.”

Sababu za kujua na kutumia jina la Mungu

  •   Mungu anaona jina lake Yehova kuwa la maana, kwa sababu alifanya lipatikane mara maelfu katika Biblia.​—Malaki 1:​11.

  •   Yesu, Mwana wa Mungu, alikazia mara nyingi umaana wa jina la Mungu. Kwa mufano, alisali hivi kwa Yehova: “Jina lako na litakaswe.”​—Mathayo 6:9; Yohana 17:6.

  •   Watu wenye wanafikia kujua jina la Mungu na kulitumia wanakamata hatua za kwanza za kujenga urafiki pamoja na Yehova. (Zaburi 9:​​10; Malaki 3:​16) Urafiki kama huo unawawezesha kupata faida kutokana na ahadi hii ya Mungu: ‘Kwa sababu ameweka upendo wake juu yangu, mimi nitamuokoa pia. Nitamulinda kwa sababu amelijua jina langu.’​—Zaburi 91:14.

  •   Biblia inasema hivi: “Kuna wale wanaoitwa ‘miungu,’ iwe wako mbinguni au duniani, kama vile kulivyo na ‘miungu’ mingi na ‘mabwana’ wengi.” (1 Wakorintho 8:​5, 6) Hata hivyo, inamutambulisha Mungu wa pekee wa kweli kwa jina lake, Yehova.​—Zaburi 83:18.

^ Watu fulani wa elimu ya Kiebrania wanapendelea kutumia “Yahweh” kama jina la Mungu.

^ Ufupisho wa jina la Mungu, “Yah,” unapatikana mara 50 hivi katika Biblia, kutia ndani matumizi ya jina hilo katika neno “Haleluya,” lenye kumaanisha ‘Musifu Yah.’​—Ufunuo 19:1.